• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

CMT YAKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO MASWA

Posted on: December 7th, 2024

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya ya Maswa.

Timu ya Menejimenti imekagua miradi hiyo tarehe 06 Desemba, 2024 na kutoa ushauri kwa wasimamizi wa miradi hiyo kuhakikisha wanasimamia kwa weredi miradi na kutoa taarifa mapema pindi wanapopata changamoto katika utekelezaji wa miradi hiyo ili changamoto hizo ziweze kutatatuliwa.

Katibu wa Kamati hiyo ambaye pia ni Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg, Masanja Kengese ametoa wito kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili wakamilishe miradi    hiyo   kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa ili ifikapo mwezi wa kwanza miradi hiyo ianze kutumika.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakandarasi hao wanaotekeleza miradi hiyo wameiomba timu ya menejimenti kuwahimiza wazabuni wanaosambaza madini ujenzi kuhakikisha wanafikisha madini ujenzi hayo katika maeneo husika ya ujenzi ili kuwarahisishia mafundi kufanya kazi kwa urahisi ili waweze kukamilisha kazi kwa muda uliopangwa.

Timu ya menejimenti imetembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya  Afisa Ugani katika  Kata ya Sengwa yenye thamani ya shs milioni 38, ujenzi wa shule mpya ya sekondari Mwabaraturu iliyopo Kata ya Mwabaraturu yenye thamani ya shilingi milioni 584.

Aidha timu imekagua mradi wa vyumba 3 vya madarasa na matunda 6 ya vyoo katika shule ya msingi Budekwa iliyopo Kata ya Budekwa yenye thamani ya shilingi milioni 88, ambapo ujenzi upo katika hatua ya ukamilishaji.

Pia wajumbe wa timu hiyo wamekagua Ujenzi wa nyumba ya walimu (2in1) shule ya sekondari Dakama yenye thamani ya shilingi milioni 100, ujezi wa nyumba hiyo upo katika hatua ya msingi, ujenzi wa jengo la Zahanati Kijiji cha Mbaragane Kata ya Mbaragane lenye thamani ya shilingi milioni 92.

Pamoja na ujenzi wa shule mpya ya sekondari katika kata ya Sukuma yenye thamani ya shilingi milioni 584 ambapo ujenzi wake upo katika hatua ya msingi.

PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA ZIARA YA CMT KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI MASWA

Timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Maswa ikikagua  ujenzi wa nyumba ya Afisa Ugani katika Kata ya Seng’wa katika ziara yao ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi  tarehe 06 Desemba 2024.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya  Wilaya ya Maswa ikikagua  ujenzi wa vyumba vya madarasa 3 na matundu ya vyoo 6 katika shule ya Msingi Budekwa iliyopo Kata ya Budekwa katika ziara yao ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi  tarehe 06 Desemba 2024.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya  Wilaya ya Maswa ikikagua  ujenzi wa shule mpya ya Sekondari katika Kata ya Mwabaraturu ikiwa ni ziara yao ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi,  tarehe 06 Desemba 2024.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya  Wilaya ya Maswa ikikagua  ujenzi wa nyumba ya mwalimu (2 in 1) katika shule ya Sekondari Dakama iliyopo Kata ya Dakama ikiwa ni ziara yao ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi  tarehe 06 Desemba 2024.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya  Wilaya ya Maswa ikikagua  ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Mbaragane kilichopo Kata ya Mbaragane  katika ziara yao ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi  tarehe 06 Desemba 2024.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya  Wilaya ya Maswa ikikagua  ujenzi wa shule mpya ya Sekondari katika Kata ya Sukuma  ikiwa ni ziara yao ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi,  tarehe 06 Desemba 2024.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya  Wilaya ya Maswa ikikagua  ujenzi wa Ofisi ya Utawala katika Kitongoji cha Ng’hami Kata ya Nyalikungu ikiwa ni ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi,  tarehe 06 Desemba 2024.



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.