• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BARAZA LA WAFANYAKAZI MASWA WAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA BILIONI 52.4

Posted on: March 4th, 2024

Baraza la wafanyakazi Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu limepitisha Rasimu ya mapendekezo ya mpango na bajeti ya shilingi bilioni 52.4 kwa mwaka wa fedha wa 2024/2025  ambapo limetoa mapendekezo katika maeneo ya kimkakati kutengewa bajetu ili kuongeza tija katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri.

Hayo yamesemwa leo katika kikako cha baraza la wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Awali akiwasilisha bajeti hiyo afisa mipango na uratibu Ndg Steven Musika amesema katika utekelezaji wa mpango na bajeti ya maendeleo wa mwaka 2024/2025 Halmashauri imekadiria kukusanya na kutumia jumla ya shilingi bilioni 52.4 ikiwa ni ongezeko la shilingi milioni 6.5 sawa na asilimia 14%.

Ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2023/2024. Ya kiasi cha shilingi bilioni 45.9  ambapo ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa fedha za mishahara ya ajira mpya na upandishaji vyeo kwa watumish.i

Aidha amesema katika mapendekezo ya mpango na bajeti  yamezingatia vipaumbele katika maeneo  muhimu ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya elimu kwa kujenga madaras 64, maabara 6, utengenezaji wa madawati 750, viti na meza 180 na ujenzi wa matundu ya vyoo 227.

Kuimalisha ukusanyaji wa mapato ambapo shilingi milioni 100 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika minada mikubwa ya Shanwa na Senani, kujenga kitega Uchumi katika eneo la MADECO,  uanzishwaji wa karakana ya matengenezo ya magari pamoja

 kuimarisha miundombinu ya afya kama vile ukamilishaji wa zahanati 4, ujenzi wa matundu ya vyoo 15 katika Zahanati 5na ukamilishaji wa vituo vya Afya 3 ili kuboresha huduma  za Afya  kwa kuhakikisha viyuo vya kutolea huduma vilivyopo vinapata dawa na vifaa tiba kwa ajili ya wagonjwa.

pia upatikanaji wa pembejeo za kilimo na mifugo, upimaji wa afya ya udongo masoko ya mazao sambamba na kuendeleza kilimo cha umwagiliaji chenye tija , kupanda miti milioni 2 ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuimarisha usafi na hifadhi ya mazingira.

“Halmashauri imetenga jumla ya shilingi milioni 191 kwa ajili ya kuboresha hali ya lishe wilayani ili kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza na utapiamlo sambamba na hilo pia imetenga shilingi milioni 327 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kutoa fursa ya mikopo nafuu ya asilimia 10% kwa shughuli za ujasiliamali.” Amesema Afisa mipango na uratibu

Akizungumza katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw. Maisha Mtipa amewataka Wakuu wa Divisheni  kuboresha mambo yote yaliyoshauriwa ili yaonekane katika bajeti zao.

Pia ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuongeza bajeti ya watumishi kutoka shilingi bilioni 24 ambayo Halmashauri ilitenga hadi kufikia shilingi bilionoi 26. Amesema

“Mhe Rais ameongeza zaidi ya bilioni mbili katika bajeti yetu kwa hiyo serikali yetu sasa hivi inajali watumishi zamani ilikuwa unatenga bilioni 24 lakini unaweza kupata bilioni 20 tunampongeza Mhe. Rais kwa kuwa anajali watumishi.” Mkurugenzi Mtendaji


“Niwaombe tu watumishi sisi ni watumishi wote tukafanye kazi kwenye maeneo yetu na tukawe wawakilishi wa wenzetu katika haya mambo kwa sababu sisi tunawawakilisha watu wengi kule waliopo, tukawaeleze miradi tunayotekeleza, iliyopo na sisi ni wasimamizi wa miradi hii tukaisimamie kwa uaminifu mkubwa.” Amesema Bw. Mtipa

Ameongeza kuwa walimu wana miradi ya madarasa na watumishi wa afya  wana miradi ya zahanati hivyo amewataka kusimamia kwa uaminifuili  ili kuwaletea  maendeleo wananchi wa Maswa na amewahasa kufanya kwa kuzingatia sheria na taratibu

Watumishi wana haki ya msingi lakini haki haiwezi kuja bila kutekeleza wajibu, kwahiyo wajibu tuufanye ibaki mwajiri au menejimenti iweze kukupa haki yako  kwa hiyo tukatekeleze kwa mujibu na tukawaambie wenzetu wakatekeleze wajibu wao katika maeneo ya kazi na changamoto zote tumezichukua  kutazifanyia kazi.mkurugenzi mtendaji

Pia Mkurugenzi Mtendaji amewataka watumishi kuhakikisha wanahamasisha suala la ukusanyaji wa mapato katika maeneo yao ili yaweze kusaidia katika masuala mbalimbali pamoja na kueleza miradi yote inayotekelezwa kwa mapato ya ndani.

Kwa upande wao wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wameshauri maeneo yote ya kimkakati yapewe kipaumbele ikiwepo maeneo ya skimu za umwagiliaji majosho, pamoja na Barabara ili kuhakikisha mapato ya Halmashauri yanaongezeka.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.