• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Afisa Lishe azitaka Divisheni zote kuwekeza katika lishe

Posted on: November 24th, 2023

Afisa lishe wa Mkoa wa Simiyu Bw. Denis Madeleke ametoa wito kwa Divisheni zote kuwekeza katika lishe ili kukabiliana na tatizo la utapiamlo na udumavu katika mkoa wa Simiyu kwa kuwa matatizo ya lishe hayaondolewi kwa maneno bali yanaondolewa kwa vitendo.

Alizungumza hayo katika kikao cha maandalizi ya mipango na bajeti za afua za lishe kwa mwaka 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na kilichohusisha Kamati ya lishe ya Wilaya pamoja na wakuu wa Divisheni na vitengo.

Afisa lishe  alisema katika Mkoa wa Simiyu tafiti zilizofanywa mwaka 2022 zinaonyesha Mkoa wa Simiyu kuna changamoto ya lishe ambapo katika watoto 100 watoto 33% wamedumaa, 68%  wanaupungufu wa damu  na 50% ya akina mama wana changamoto ya lishe.

“Tukiwekeza katika huduma za mama, tukawekeza katika huduma za vijana tuna uwezo wa kuondoa matatizo ya utapiamlo na njia pekee inayotumika zaidi na  inayofanya vizuri ni siku ya afya na lishe ya kijiji tukiweza bukoresha siku ya afya na lishe ya kijiji tunaweza tukaboresha huduma  na mwisho wake tukaondoa tatizo la utapiamlo.” Alisema Afisa lishe Mkoa

Aliongeza kuwa ili kukabiliana na tatizo la utapiamlo mkali vipaumbele vya mkoa ni kuhakikisha huduma hizo  Zinatolewa katika  Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya na Zahanati zote zitatoa matibabu ya kawaida ya utapiamlo pamoja na kutenga  fedha kwa ajili ya kukusanyia taarifa katika jamii.

Pia Bw. Madeleke  alisema  elimu inatakiwa  itolewe zaidi kwa akina mama kuhusu umuhimu wa kutumia  chumvi za madini joto kwa sababu itamsaidia  mtoto aliyepo tumboni kutengeneza ukuaji wa ubongo wake vizuri pamoja na utoaji wa dawa aina ya FEFO na Foliki Asidi ambayo itawasaidia akina mama kuongeza damu ndani ya miezi mitatu tangu kushika mimba.

Afisa lishe alisisitiza dawa hizo zitasidia akina mama wengi katika mkoa wa simiyu kuepukana na kujifungua watoto wenye vichwa vikubwa pamoja na mgongo wazi, sambamba na hilo elimu ya lishe itolewe vizuri mashuleni ili kusaidia utekelezaji wa afua za lishe.

Kwa upande wake Afisa lishe wa Wilaya ya Maswa Ndg Abel Gyunda  alisema Halmashauri imetenga mpango na bajeti ya  kiasi cha shilingi milioni 127 kwa ajili ya utekelezaji wa afua za lishe katika Divisheni za Halmashauri na vyanzo mbalimbali kwa ajili ya watoto chini ya miaka 5 ili kusaidia kukuabiliana na utapiamlo na udumavu.

Nae Mganga Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dr. Hadija Zegegga alisema ili Wilaya ionekane imefanya vizuri ni lazima fedha zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za lishe zitumike.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.