• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ZOEZI LA UCHAGUZI WILAYANI MASWA LAFANYIKA KWA AMANI

Posted on: November 27th, 2024

Zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Wilaya ya Maswa limefanyika kwa Amani ambao viongozi mbalimbali wameendelea kutoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kupiga kura ili kuchagua viongozi watakao waongoza katika maeneo yao.

Akizungumza baada ya kupiga kura katika kituo cha Kitongoji cha Mwatonja Kata ya Nyalikungu Mkuuwa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kupiga kura katika vituo 510 vilivyopo katika maeneo yao.

Aidha mhe Kaminyoge amesema kuwa zaidi ya wananchi laki moja na elfu hamsini na tano (155,000) wamejiandikisha kupiga kura hivyo amewataka wananchi wote waliojiandikisha kwenda kupiga kura ili kuchagua viongozi ambao watawaongoza.

“Tunataka wananchi wote waliojiandikisha laki moja na hamsini na tano (155,000) wakapige kura lengo lake na madhumuni yake ni kwamba viongozi watakaochaguliwa wawe viongozi ambao wamechaguliwa na wananchi walio wengi.”

Kwa upande wake Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndugu Maisha Mtipa ambaye amepiga kura katika kituo cha Uwanja wa Ndege Kata ya Sola ambapo baada ya kupiga kura amezungumza na waandishi wa habari na kuwaeleza kuwa maandalizi ya uchaguzi huo yameenda vizuri kwa kuwa hakuna malalamiko yoyote yaliyojitokeza na vituo vyote vimefunguliwa saa mbili asubuhi ambapo wananchi tayari wameanza kupiga kura.

Pia akatumia wasaha huo kuwaomba wananchi “nawasihi wananchi wajitokeze waweze kupiga kura waweze kuchagua viongozi wao katika maeneo yao husika”

Pia ameongeza kuwa katika zoezi hilo wananchi wenye mahitaji maalumu wamepewa kipaumbele wanapokuta foleni ambapo wanakwenda moja kwa moja kupiga kura.

Nae Naibu Waziri Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki Mhe. Stanslaus Nyongo amepiga kura katika kituo cha Uwanja wa Ndege Kata ya Sola Wilayani Maswa ambapo amesema katika kituo alichopigia kura hali ya usalama ni shwari na zoezi linaendelea vizuri.

Pia Mhe Nyongo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuchagua viongozi hao kwa kuwa muda uliobaki ni mchache.

Kwa upande wao wananchi wa Wilaya ya Maswa wamewapongeza wasimamizi wa uchaguzi kwa kuweka utaratibu mzuri wa kupiga kura kwasababu wananchi hao wamesema wametumia muda mchache kupiga kura na kuondoka kuendelea na majukumu yao.

Picha mbalimbali katika matukio ya leo



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.