• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wanawake/ akina mama wafaidika na Elimu ya matumizi ya mlo kamili

Posted on: March 1st, 2023

Akina mama Ipililo wapata elimu ya namna ya kutumia mlo kamili kwa ajili ya watoto wa miaka 0-5 kwa kufundishwa namna ya kupika uji uliozingatia makundi matano  ya vyakula.

“Lishe iliyobora ndio afya ya binadamu tunazungumzia lishe kwa watoto kwa sababu akili inatengenezwa wakati wa utoto usije ukasema mtoto wa mtu fulani ana akili nzuri au anafanya vizuri darasani kwa sababu ya lishe bora, sio bora lishe”

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mpollo Adorat aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya  katika kilele cha wiki ya unyonyeshaji duniani pamoja na siku ya afya na lishe ambayo imefanyika leo tarehe 1 machi 2023 katika viwanja vya  Kituo cha Afya Ipililo  kilichopo Kijiji cha Ipililo Kata ya Ipililo.

Dkt Adorat amesema katika Mkoa wa Simiyu udumavu upo kwa asilimia 33% hivyo serikali chini ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan imempa dhamana Mkuu wa Wilaya kusimamia suala zima la afya ili kuondoa udumavu nchini Tanzania ili watoto wote kuanzia miaka 0-5 wawe safi.

Aidha, Mganga Mkuu amewasisitiza akina mama kuwa jukumu la kulisha watoto ni la kwao hivyo akina mama hao wanatakiwa kuwapa watoto wao mlo kamili ambao unahusisha makundi yote ya vyakula kwa sababu Maswa ina nyakula vya kutosha ambavyo vitamsaidia mtoto kuwa na afya bora ili kuepuka utapiamlo unaosababisha udumavu.

Kwa upande wake Afisa Lishe Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Gyunda  ametoa elimu kwa akina mama hao ya  namna ya kutumia mlo kamili kwa ajili ya kuwapa watoto wao kwa kuzingatia makundi matano ya vyakula ambayo ni vyakula vya nafaka, ndizi na mizizi, vyakula vya jamii ya mikunde na nyama, mbogamboga zote, matunda pamoja na sukari, mafuta, asali na chumvi.

Pia Afisa Lishe amesema makundi hayo matano ya vyakula yatamsaidia mtoto na mama mjamzito kuwa na nguvu, kuongeza kinga mwilini na kutoa vitamini, kuimarisha mwili pamoja na kuupatia mwili nishati ili kuepukana na kupata maradhi mbalimbali.

Ameendelea kusisitiza kuwa maziwa ya mama ya mwanzo ndio chanjo ya kwanza ya mtoto kwa kuwa yana mlo kamili ambao unajumuisha makundi yote ya vyakula ambavyo ni   wanga, protini, madini, vitamini vitakavyomsaidia mtoto kuwa na akili na afya nzuri ili kuepukana na maradhi mbalimbali.

Diwani wa Kata ya Ipililo Mhe: Sayi Samwel Maige amewashukuru viongozi wote wa Wilaya ya Maswa kwa kupeleka Elimu hiyo ya lishe bora katika kata yake na amewaomba akina mama wote kusikiliza kwa makini Elimu hiyo ili ikawasaidie watoto wao.

Nae Afisa Tarafa wa Tarafa ya Mwagala Ndg. James Hongoli amesema maelekezo ya Mkuu wa Wilaya ni kuhakikisha watoto, akina mama na wananchi wote katika kila Kijiji na Kata wanapata Elimu ili iwasaidie katika kuboresha afya za familia zao.

"Serikali kwa ujumla wake inaamini kabisa wananchi wanazalisha vyakula mbalimbali iIa sasa namna ya kuviandaa vile vyakula kutengeneza mlo kamili hapo ndio pana shida”  amesema Hongoli.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Usawa wa kijinsia jinsi unavyoathiri upatikanaji wa huduma za Afya ya uzazi na Ujinsia miongoni mwa Vijana Balehe

    August 06, 2025
  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.