• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

Posted on: July 17th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amewataka wananchi wa Maswa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ili waweze kupata vitambulisho ambavyo vitawawezesha wananchi hao kupata haki yao ya  msingi ya kikatiba ya  kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka .

Pia ameongeza kuwa zoezi hilo litawahusu wananchi wote ambao wamefikisha umri wa miaka 18, waliopoteza vitambulisho pamoja na wananchi  waliohama eneo walilojiandikisha wakati wa kupiga kura mwaka 2020.

Mkuu wa Wilaya amesema hayo wakati wa ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Kijiji Cha Shinyangamwenge Kilichopo Kata ya Dakama tarehe 17 Julai 2024.

"Wale ambao walikuwa hawajafikisha miaka 18 sasa ni wakati wao wa kwenda kujiandikisha ili wawemo katika daftari la kudumu la wapiga kura  ili mwaka 2025 wakaweze kupiga kura lakini pia ni kwa wale ambao wamehamia kutoka  sehemu nyingine,

mfano wametoka Mpanda  Katavi na Rukwa wamehamia Shinyangamwenge  sasa ili uweze kupiga kura unatakiwa ujiandikishe hapa na  taarifa zako wakati wa kupiga kura zitakuwa hapa." Mhe Kaminyoge

Pia Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa wananchi  ambao wataboresha taarifa zao pindi zoezi hilo  litakapotangazwa kuanza kuhakikisha  wanakwenda na vitambulisho hivyo vya mpiga kura  ili taarifa hizo ziweze kuboreshwa.

Katika hatua nyingine Mhe Kaminyoge amewaomba wananchi kuwalinda watoto wenye ulemavu wa ngozi ili wasipate madhara kutokana na mila potofu zinazofanywa na wagaga wa kienyeji ambao hawana vibali kutoka ofisi ya Mkurugenzi kupitia kwa mganga Mkuu wa Wilaya ambao wanatumia lamli chonganishi.

"Wale waganga wa kienyeji ni wale waganga ambao hawana vibali wanapiga lamli chonganishi mtu anakwenda anasema ili uwe tajiri unatakiwa ufanye moja mbili tatu na mtu akisikia utajiri anaondoka anaenda kutekeleza la kutekeleza anadhuru miasha ya mtu, utajili asipate, mtu anakufa, wananchi tunaomba walindeni albino kwa nafasi zenu."  Amesema Mkuu wa Wilaya

Katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya amesikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi zikiwemo za afya, maji, vitamburisho vya NIDA pamoja na elimu.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.