• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Walimu wa shule za msingi Maswa wapongezwa

Posted on: November 29th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Maswa chini ya usimamizi wa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji imefanya sherehe za kuwapongeza Walimu wote wa shule za Msingi Wilayani hapa kutokana na ufaulu mzuri walioupata mwaka huu 2019. Sherehe imehudhuliwa na wadau mbalimbali wa elimu ikiwa ni pamoja na Katibu wa CWT Taifa ambaye alikuwa Mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Maswa, Wenyeviti wa  CWT mikoa ya Mara, Shinyanga, Kigoma na Simiyu, Madiwani wa Halamashauri ya Wilaya ya Maswa, Mbunge wa Maswa Mashariki na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo na Muwakilishi wa  Mbunge wa Maswa Magharibi, Wadau mbalimbali wa Elimu Wilayani Maswa, Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Walimu wote Wilayani Maswa, Wakuu wa Wilaya Mkoa wa Simiyu na Wakurugenzi Watendaji Wilaya / Mji wa Mkoa wa Simiyu.

 Katika sherehe hii matukio mbalimbali yamefanyika ikiwemo na;

Kukabidhi kiwanja kwa Chama cha Walimu kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha Mikate inayotokana na unga wa viazi lishe.

Imefanyika harambee ya kuchangia ujenzi wa Nyumba  za walimu na ukamilishaji wa nyumba  za walimu ambazo zmeshaanza kujengwa huko katika shule za Jihu, Busamuda, Jilago na Buhangija ambapo Pesa kiasi cha Tsh. 32,700,000/= kimepatikana na Saruji mifuko 265 imepatikana.

Umefanyika uzinduzi wa mfuko wa kusaidia Walimu ambapo kwa kuanza kiasi cha Tsh.30,000,000/= kimepatikana kwa ajili ya kutunisha mfuko huo ili walimu waweze kukopeshwa kwa riba nafuu na kuepuka kugawa kadi zao za benki kwa wakopeshaji wadogo wadogo. Mfuko umezinduliwa rasmi na wadau wafuatao wametunisha mfuko kwa kuchangia kiasi cha fedha; Chama cha Walimu Tanzania CWT wamechangia Tsh. 8,000,000/=, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Tsh. 15,000,000/= na Mhe. Mbunge wa jimbo la Maswa Mashariki Tsh. 6,000,000/=.

Mgeni rasmi amekabidhi zawadi kwa shule 5 zilizofanya vizuri sana ikiwa ni cheti na pesa taslimu tsh.500,000/= kwa kila shule na amekabidhi majiko ya gesi kwa shule zote za Msingi ikiwa ni ishara ya kuzindua unywaji wa Chai kwa walimu ndani ya mazingira ya shule.

Akihutubia hadhara hiyo Mgeni rasmi amewaasa walimu kufanya kazi kwa bidii bila kuchoka ikiwa ni sambamba na kutunza nidhamu na maadili ya ualimu. Amesema matatizo yote ya walimu yanajulikana hivyo basi mazungumzo na serikali yanaendelea ili yote yaweze kutatulika ikiwa ni pamoja na waraka ambao ulitoka na kuwataka walimu wote wanaotoka masomoni wasipande madaraja yao wanayostahili.

Pamoja na changamoto hizo hakuwa nyuma kuishukuru Serikali kwa hatua inayochukua pale changamoto zinapojitokeza ikiwa ni pamoja na kupandisha madaraja na kulipa malimbikizo ya walimu hasa malimbikizo ya mishahara.

Amesema wapo watumishi wengi ambao hawakupanda madaraja kutokana na kutokuwepo kwenye mpango, tatizo hili linatatuliwa kwa ushirikishwaji wa chama cha walimu na ofisi ya utumishi kwa kutengeneza mpango kazi. Amesisitiza sana Walimu kujiunga na benki ya Mwalimu ili waweze kukopesheka kiurahisi kupitia mfuko uliozinduliwa.

Aidha ameshukuru sana kwa ushirikiano wa viongozi mbalimbali wa Mkoa na Wilaya kwa Walimu hasa kwa kubuni jambo jema litakalo inua uwajibikaji kwa walimu kwani sherehe hii ni ya mfano Tanzania.

Sambamba na hayo CWT imetoa Tsh.10,000,000/= kwa ajiri ya usafiri kuwarudisha shuleni kwao walimu wote waliohudhulia sherehe hii.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.