• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

Posted on: March 26th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imekabidhi mkopo wa  shilingi milioni 173.6 kwa  vikundi  15 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa awamu ya kwanza  ikiwa ni sehemu ya asilimia kumi ya mapato yake ya ndani katika mwaka wa fedha unaoendelea.

Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bi.  Basila Bruno wakati wa hafla ya  kukabidhi  hundi kwa vikundi vya wanawake, vijana  na watu wenye ulemavu  katika ukumbi wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa  Maswa tarehe 26 Machi 2025.

Amesema katika awamu ya kwanza ya  mkopo huo vikundi vya wanawake 7 vimekopeshwa shilingi milioni 78.9, vikundi vya  vijana 5 vimepokea milioni  81, pamoja watu wenye ulemavu vikundi 3 vimekopeshwa milioni 13.7.

Pia Bi. Bruno ameongeza kuwa Halmashauri imeweza kutenga na kutoa mikopo kwa makundi yote ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kuongeza kipato kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kutokana na miradi yao na hivyo kuchangia pato la Halmashauri ya Wilaya na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw.  Robert Urassa amewataka wanufaika wote wa mikopo kuhakikisha fedha hizo wanazozipata zikafanye shughuli inayotakiwa na kuweza kuzilejesha kwa wakati.

“Wanaohitaji mikopo hii ni wengi na nyie mmebahatika kupata mikopo hii kwa awamu ya kwanza tunahitaji mkafanye kile mlichotarajia kukifanya ili mrejeshe fedha hizi kwa wakati ili wanawake wengine, vijana na watu wenye ulemavu katika Halmashauri yetu ya Maswa waendeleee kunufaika.”amesema Bw. urassa

Pia ametoa wito  kwa vikundi hivyo kuhakikisha vinatakeleza malengo yaliyokusudiwa katika biashara   kwa kuwa Halmashauri imewapa mitaji ili waweze kujiendesha na amesisistiza kuwa zoezi hilo ni endelevu ambapo awamu ya pili ya utoaji wa mikopo itaendelea katika vikundi vingine vilivyoomba.

Akikabidhi hundi kwa vikundi, Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mh. Vincent Anney amesema fedha hizo sio fedha za kunywea pombe, kununua shamba  mikopo hiyo ni kwa ajili ya kwenda  kuanzisha biashara ndogondogo ambazo zitakwenda kuwapa mtaji ili baadae wajitegemee.

“Naomba sana tumsaidie Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwa yeye mwenyewe  aliamua kuboresha mfumo wa utoaji wa mikopo ya asilimia kumi kwa nchi nzima kwa kutunga sheria na kubadilisha utaratibu, Dkt Samia anataka watanzania wajikomboe ili wajikomboe fedha hii ya mikopo lazima ilejeshwe na ili irejeshwe unatakiwa uishi kwenye mpango kazi wako wa biashara.”  ameeleza Dkt Anney

Pia ametoa wito kwa vikundi vyote kuhakikisha wanarejesha mikopo hiyo kwa wakati bila kuongeza muda kwa kuweka mpango kazi wa kulipa mkopo huo  ili watu wengine waweze kupata fursa ya kukopeshwa mikopo hiyo.

Aidha amewapongeza wanawake wote kwa kuwa mstari wa mbele kulipa mikopo na kuwataka vijana kuepuka tabia za kutokulipa mikopo hiyo kwa wakati.

Pia amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji  kuwasilisha majina ya vikundi vyote vinavyodaiwa katika ofisi ya  TAKUKURU ili watu hao wafikishwe mahakamani ili fedha hiyo iweze kurejeshwa.

Kwa upande wa vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo vimeishukuru serikali ya awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kurejesha mikopo hiyo kwa kuwa sasa itawasaidia kufanya shughuli ambazo wamekusudia na kuahidi kurejesha kwa wakati mikopo hiyo ili na wengine wapate mikopo hiyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.