• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Vijana wa Kike chini ya mradi wa Vijana Tunaweza wakutana na viongozi wa Serikali

Posted on: September 24th, 2021

Vijana wa Kike chini ya Mradi wa Vijana tunaweza unaofadhiliwa na shirika la UNFPA na kutekelezwa na Restless Development wamekutana na Viongozi wa serikali Wilayani Maswa leo tarehe 24/09/2021.

Mradi wa Vijana Tunaweza ni mradi wa kuwezesha wasichana unaotekelezwa  na Restless Development wenye lengo la kupunguza visababishi  vinavyopelekea wasichana kuingia kwenye maambukizi ya VVU na UKIMWI, mimba zisizo tarajiwa ukatili wa kijinsia na ndoa za utotoni. Vijana tunaweza hutumia mbinu shirikishi ambayo inapambania  elimu ya makuzi, haki na afya ya uzazi uwezeshaji wa kiuchumi  na kuwajengea kujiamini katika kufanya maamuzi yanayogusa maisha yao.

Ndani ya Wilaya ya Maswa mradi huu ulianza mwaka 2021 mwezi 3 na unawafikia mabinti wenye uzao mmoja 30 wakiwa wameunganishwa  kwenye vikundi vidogo 3 ndani ya kata ya Lalago, Badi na Sola hapa Wilaya ya Maswa. Katika kufanikisha  utekelezaji wa mradi huu, shughuli mojawapo  ni vijana kukutana na viongozi wa Serikali na wadau wengine mbalimbali ambao wanamchango mkubwa katika kufanikisha maendeleo ya vijana  na kuwasilisha maoni na mapendekezo, kujadiliana nao katika ufumbuzi wa changamoto mbalimbali na kutengeneza mahusiano mazuri na endelevu.

Kati ya Mambo yaliyojadiliwa na vijana wa Kike Kutoka Katika Kata ya Badi, Sola na Lalago ni pamoja na :-

  1. Huduma rafiki ya afya ya uzazi kwa vijana
  2. Ukatili wa kijinsia
  3. Uwezeshaji wa wanawake na wasichana kiuchumi
  4. Ushiriki na ushirikishwaji katika maamuzi

Kaimu Mkurugenzi katika kuhitimisha aliwahakikishia vijana kuwa  kupitia katika vikundi  vyao watapata mikopo ya kisheria itolewayo na Halmashauri kwa  Vijana , Wanawake na Watu wenye ulemavu, pia aliwaagiza watendaji wote walio chini yake kuhakikisha wanasikiliza kero za Vijana wa kike na kuzitatua pindi zitokeapo ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha katika vikao ili watoe maoni  na mapendekezo yao.

Aidha Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji aliwashukuru sana  Viongozi wote walioanzisha Mradi huu wa Vijana tunaweza kwa nia yao njema ya kuwajengea vijana wa kike uwezo wa kujiamini na kuwainua kiuchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.