• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Uboreshaji wa matumizi ya Ardhi kukuza uchumi Maswa

Posted on: March 2nd, 2023

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeendelea kuboresha sekta ya ardhi kwa kuandaa mpango wa matumizi sahihi ya ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa yenye lengo la upangaji unaoainisha matumizi sahihi ya rasilimali ardhi kulingana na mahitaji ili kuongeza tija katika uzalishaji.

Hayo yameelezwa na Afisa Mipango Miji Mkuu kutoka Wizara ya Ardhi  Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ndg. Aristides  Mulokozi wakati akitambulisha mradi huo kwa Madiwani, kamati ya ulinzi na usalama, wataalamu wa Halmashauri na Watendaji wa Kata  katika kikao cha baraza la madiwani lililofanyika leo tarehe 2 March 2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Ndg. Mulokozi amesema Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ni miongoni mwa Halmashauri  sita zilizopata fursa ya kupitiwa na mradi huo kwa sababu ya ongezeko la idadi ya watu, kukua kwa sekta za miundombinu pamoja huduma za kiuchumi na kijamii.

Mpango huo upo kisheria kwa ajili ya  kutatua changamoto kwa kuzuia uharibifu wa ardhi na  rasilimali zake, kulinda maeneo ya uwekezaji na kuratibu mipango ya maendeleo ya kisekta inayohusiana na upangaji wa matumizi ya ardhi  na hivyo kupelekea  matumizi endelevu ya rasilimali za ardhi katika Wilaya.

Aidha, ndg. Mulokozi amesema kuwa mpango huo hautajikita katika mambo ya ardhi peke yake utajumuisha maeneo mengine kwa sababu mradi huo utapita kila Kata kuchukua taarifa za kidemografia na kijamii, pamoja na uboreshaji wa Ofisi za ardhi za Wilaya na za vijiji pamoja na kutoa hati za kimila.

Ameongeza kuwa mradi huo utadumu kwa muda wa miaka 20 hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi kutokana na mipango ya Halmashauri ya Wilaya  kuainisha miradi ya maendeleo inayopaswa kutekelezwa na pia itasaidia kutatua migogoro ya ardhi.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ndg. Simon Berege ameishukuru Wizara ya Ardhi, Nyumba, na maendeleo ya makazi kwa kuleta mradi huo ambao utaleta mabadiliko makubwa katika Wilaya ya Maswa na kutatua matatizo ya kijamii na migogoro mbalimbali.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.