• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Shule 20 bora zapewa zawadi ya majiko maswa

Posted on: March 12th, 2018

Leo tarehe 12/3/2018 kulikuwa kikao cha Wadau wa elimu Wilayani Maswa ambacho Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka. Kikao hicho kimejumuisha Waheshimiwa Madiwani, Walimu Wakuu, Wakuu wa Shule, Maafisa Elimu Kata, Wenyeviti wa Kamati za Shule, Wakuu wa Idara na Walimu.Katika kikao hicho Mgeni rasmi ametoa zawadi za majiko ya gesi kwa shule 20 zilizofanya vizuri kwenye mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi darasa la saba Mwaka 2017, ametoa vyeti kwa Wadau mbalimbali wanaochangia shughuli za maendeleo ya Elimu, ametoa vyeti kwa shule 10 zilizofanya vizuri mtihani wa Mock na shule 10 zilizofanya vibaya mtihani wa Mock. Amepokea na kugawa magunia ya mahindi kwa shule za Msingi za Wilaya ya Maswa yaliyotolewa na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuchangia chakula cha Wanafunzi shuleni. Aidha amefungua mashine za kutolea nakala aina ya RISO zitakazotumiwa kwa ajili ya kudurufu mitihani na kazi mbalimbali za kitaaluma ili kusaidia kupunguza garama za uendeshaji wa Shule Wilayani Maswa.

Sambamba na utoaji zawadi ametoa hotuba juu ya manufaa ya elimu kwa jamii ili kuleta mapinduzi ya maendeleo. Amesema ilikuwa na maendeleo katika  eneo lako lazima elimu iwe kipaumbele katika eneo hilo, kwa kusisitiza amese "tazama nchi zilizoendelea ndizo zina Vyuo bora, na hata miji iliyoendelea ndiyo ina vyuo bora". Katika hili Wazazi na Walezi wamehimizwa kusomesha watoto wao ili kuandaa misingi mizuri kwa ajili ya maendeleo ya Wilaya ya Maswa. Ili kukabiliana na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia kia mzazi au mlezi ajiandae kumuelimisha mwanaye.

Kuhusu suala la chakula amehaidi kwa kushirikiana na Afisa Elimu wa Mkoa atakutana na Wenyeviti wa Kamati za shule ili wakahamasishe wazazi kuchangia chakula ili watoto wasome vizuri.

Aidha amewataka wazazi kuwasimamia watoto wao ili wasome na siyo kutoa lawama kwa walimu na hali matatizo yanaanzia kwenye familia. Hii itasaidia kila mtu kusimamia majukumu yake ya kuendeleza suala zima la elimu. Kila Mzazi au Mlezi ahakikishe mtoto ananidhamu anaenda shule na Mwalimu ahakikishe anafundisha wanafunzi.

Amewahasa wazazi na walezi wanaowakataza watoto kwenda shule au kufanya vibaya mitihani yao ya mwisho kutoendelea na tabia hiyo mbaya maana inarudisha maendeleo nyuma.

Ametoa maamuzi kuwa wanafunzi wote wa kidato cha sita Mkoani Simiyu kuanzia tarehe 3/4/2018 hadi 17/4/ 2018 watakuwa kwenye makambi ya kujifunzia. Wasichana watakuwa shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na Wavulana watakuwa Shule ya Sekondari Binza.

Amemuelekeza Mkurugenzi Mtendaji kuwapa zawadi watumishi waliofanya vizuri majukumu yao na kuleta tija kwa jamii na taasisi yao siku ya maadhimisho ya mei mosi

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.