• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Serikali imetoa Shilingi bilioni 7,155,691,986/= kutekeleza miradi ya maendeleo Maswa

Posted on: May 12th, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Simon Berege ameishukuru serikali ya   Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kiasi Cha shilingi bilioni 7,155,691,986/= kutoka serikali kuu kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akisoma  taarifa   katika kikao Cha Baraza la madiwani Cha robo ya tatu kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Berege amesema katika robo ya tatu serikali imetoa Fedha kwa asilimia mia moja katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na tayari miradi hiyo inaendelea mingine inaanza ikiwepo ujenzi wa matundu ya vyoo 41 katika shule sita, ujenzi wa shule tatu mpya, ununuzi wa vifaa tiba na mingine mingi inatekelezwa katika sekta za Elimu na afya.

Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita imetoa shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya la  Halmashauri  ambalo litajengwa Kata ya Nyalikungu katika kitongoji cha Ng'hami

Ndg Berege ameeleza kuwa Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameipatia Fedha Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa ajili ya ujenzi wa VETA mpya kubwa na ya kisasa ambayo itajengwa katika Kata ya Sola karibu na Shule ya msingi Sola na itasimamiwa na chuo Cha maendeleo ya wananchi Malampaka.

Aidha amesisitiza kuwa wataalamu tayari walifika eneo la mradi na kuridhishwa na eneo hilo ambapo amesema matangazo tayari yameshatoka ili wazabuni wapatikane pamoja na wajenzi ili ujenzi uanze.

"Sisi watendaji  na madiwani wote tutatoa ushirikiano, itakuwa ni suluhisho kubwa kwa vijana wetu kwa sababu mradi mkubwa sana na utaleta mabadiliko makubwa sana katika Halmashauri yetu" amesema Mkurugenzi Mtendaji.

Nao madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wamempongeza Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kuleta Fedha za miradi ya maendeleo na wameahidi kumuunga mkono kwa kusimamia miradi mbalimbali katika kata zao.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa wilaya ya Maswa Ndg Agness R  Alex akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge katika salamu za serikali amesema msimu wa pamba umefunguliwa hivyo amewataka wanunuzi kufuata Sheria na taratibu za ununuzi wa pamba na amewataka wananchi wa Maswa kuhakikisha pamba yote inanunuliwa katika maeneo yaliyotegwa kwa ajili ya kuuzia pamba, na yeyote atakayetorosha pamba kwenda nje ya Maswa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Pia ametoa wito kwa madiwani pamoja na wataalamu wa Halmashauri kusimamia miradi ili ikamilike kwa wakati na kujali thamani ya Fedha.

" Kila Mhe Diwani kwenye eneo lake ahakikishe miradi iliyopo kule inakamirika na kutekelezwa kwa wakati, yale ambayo wananchi wanatakiwa kuyafanya wayafanye  tuwahamasishe wananchi wafanye,  na yale ambayo sisi serikali tunatakiwa kufanya tuyafanye, sisi kama watendaji tunatakiwa tuyafanye kwa wakati na mwisho wa siku thamani ya Fedha inaonekana na mradi unaonekana"  amesema Katibu Tawala.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.