• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC KIHONGOSI AIPONGEZA MASWA KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: July 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Kenani Kihongosi ametoa pongezi kwa watumishi wa Maswa kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika wilaya hiyo.

Mhe Kihongosi ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo  aliyoifanya katika Wilaya ya Maswa

“Watumishi wa Maswa hongereni sana mzidi kutoa ushirikiano kwa Mkurugenzi wenu, Mkuu wa Wilaya na vyombo vyote vilivyopo hapa, kila mmoja ana wajibu wa kuitumikia nchi hii tumepewa vipande, tumepewa dhamana, tumepewa kazi na tuliomba kazi na Mungu akatujalia tukapata kazi, wajibu wetu kila mmoja akawajibike ajue ana deni.”

Pia amewataka watumishi hao kutendea kazi dhamana walizopewa kwa kuwatumikia wananchi ambao wanalipa kodi na fedha hizo zinatumika katika utekelezaji wa miradi hivyo amewaomba  watumishi  hao kuwajibu katika  usimamizi wa  miradi hiyo kwa weredi.

Akiwa Wilayani Maswa Mkuu wa Mkoa amekagua ujenzi wa bweni la wasichana katika shule ya sekondari Mwagala iliyopo kata ya Lalago ambapo Serikali kuu imetoa kiasi cha shs milioni 156 na mradi huo upo katika hatua ya ukamilishaji.

Pia amekagua mradi wa ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita laki mbili na mfumo wa usambazaji maji katika vijiji vya Zanzui, Malita na Mwabujiku wenye thamani ya shs bilioni 1.5, ujenzi wa kiwanda cha mtu binafsi cha kuchakata pamba kilichopo eneo la Nghami Kata ya Nyalikungu wnye thamani ya shs bilioni 1.5.

Aidha mkuu wa mkoa amekagua ujenziwa majengo yamionzi,maabara, kichomea taka na wodi binafsi pamoja na ukarabati wa mfumo wa umeme  katika hospitali ya maswa yenye thamani ya shs milioni 900 fedha kutoka serikali kuu ujenzi wa barabara ya  kiwango cha lami yenye  urefu wa mita 850 kutoka posta hadi njiapanda (Ikulu Road).

 Pamoja na mradi wa  kiwanda cha kufyatua tofari cha  kikundi cha vijana wa Upendo Shanwa kilichopata mkopo wa shs. Milioni 9.4 kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kilichopo katika eneo la viwanda Ng’hami Kata ya Nyalikungu.

Miradi hiyo ikikamilika itataua changamoto mbalimbali  katika wilaya ya maswa zikiwepo za ajira, afya elimu na usafirishaji.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.