• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mwenyekiti UWT Taifa aridhishwa na miradi ya maendeleo Maswa

Posted on: September 18th, 2023

Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Chatanda amempogeza Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa Fedha nyingi hususani katika ujenzi wa shule za Msingi na Sekondari pamoja na miundombinu mingine ambayo inatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

"Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa Fedha nyingi ili watoto wetu waweze kusoma, jukumu letu sisi wazazi ni kushirikiana na serikali kuhakikisha kwamba mnawaandaa watoto waweze kwenda shule sio serikali ijenge majengo halafu baadhi ya watoto hawaendi shule, watoto wote wenye umri wa kwenda shule kuanzia hawa wadogo wa kwenda shule kuanzia hawa wa chekechea pale wamejengewa shule nzuri sana ya chekechea wapelekeni watoto shule". Amesema Ndg Chatanda.

Amezungumza hayo kwa nyakati tofauti wakati akikagua na kuongea na wananchi katika maeneo mbalimbali ya miradi ya maendeleo aliyoitembelea leo tarehe 17.09.2023 katika Wilaya ya Maswa na kuridhishwa na miradi hiyo ambayo imetekelezwa kwa ufanisi.

Aidha Mwenyekiti wa UWT Taifa ametoa wito kwa jamii kuwapeleka watoto wa kike shule na kuachana na Mila potofu za kuwaozesha pindi tu wanapofika hatua ya kubalehe hivyo amewasisitiza wazazi kuwa urithi wa mtoto wa kike ni kufika chuo kikuu na hata kama atashindwa kufaulu darasa la saba au kidato cha nne au sita serikali kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi inajenga vyuo vya VETA kila Wilaya lengo ni kuwasaidia vijana na mabinti kupata Elimu ya ufundi ambayo itawasaidia kupata maarifa ya kujitegemea na kuacha kuwa tegemezi.

Pia Ndg Chatanda amewaomba wazazi kuwasimamia vizuri watoto kwa kuwa kumekuwa na mmomonyoko mkubwa wa maadili kwa watoto hivyo amewasihi wazazi kukaa na watoto wao kwa kuwaelekeza na kuwalea watoto katika maadili mema na ameiomba jamii kuwafichua watu wote wanaowafanyia ukatili watoto hasahasa wanafunzi ili waweze kufikishwa kwenye vyombo vya Dora.

Pia amewataka wananchi wote kupima afya zao katika vituo vya kutolea huduma ya afya wakiwepo akina mama wajawazito ili kuepuka matatizo ya vifo vya uzazi vinavyoweza kutokea pindi ambapo mama amejifungulia nyumbani.

Ameongeza kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kupitia mama Samia Suluhu Hassan imeandaa utaratibu mzuri kwa ajili ya mikopo ya asilimia kumi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu nia ya serikali ni kuwaondoa wanawake katika mikopo ya kausha damu na mwendo kasi kwa kuwa mikopo ya serikali haitakuwa na riba na itakopeshwa kupitia benki ya NMB na CRDB na itatolewa kwa mtu mmoja mmoja atakayetaka kukopa.

Akiwa Wilayani Maswa Ndg Chatanda ametembelea miradi mbalimbali ambapo ametembelea na kukagua Shule mpya ya Majengo iliyopo katika Kata ya Shishiyu ambayo ujenzi wake upo katika hatua ya ukamilishaji ambapo kiasi cha shilingi milioni 348,500,000/= kimetolewa na serikali kupitia mradi wa BOOST, amekagua ujenzi wa Kituo cha afya kilichopo Kata ya Shishiyu chenye thamani ya Shilingi milioni 500,000,000/=,  Zahanati ya Barikiwa, Jengo la dharura katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa ambalo lilipata Fedha kiasi cha shilingi milioni 300,000,000/= kutoka serikalini kupitia Fedha za Uviko19 lengo likiwa ni kuboresha huduma zote za matibabu ikiwepo ya dharura.

Pia ametembelea shule kongwe ya Shanwa ambayo ilianzishwa mwaka 1928 na kuona ukarabati uliofanyika ambapo shilingi milioni 100,000,000/= zilitolewa na serikali kuu kwa ajili kukarabati vyumba vya madarasa 10 na ofisi 4 lengo likiwa ni kuboresha Mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi pamoja na kutembelea na kukagua kiwanda cha Sola ambacho kinajishughulisha na uchakataji wa zao la Pamba ambapo serikali ilikifufua  kiwanda hicho kwa kutoa kiasi cha shilingi bilioni 5 kutoka benki ya maendeleo TDB ambapo kinafanya kazi mpaka sasa .


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.