• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MUAC kutambua watoto wenye matatizo ya lishe

Posted on: March 4th, 2023

Watendaji wa Kata na waganga wa tiba asilia wamepata elimu ya matumizi ya vifaa maluum vya kuwapima watoto katika maeneo yao na kuwapa uelewa watendaji wa Kata wanapopewa taarifa na watendaji wa vijiji waweze kubaini watoto wenye udumavu, ukondefu pamoja na uzito pungufu ili wapelekwe hospitali kwa ajili ya matibabu.

Pia amesema waganga wa tiba asilia na watendaji wa Kata wanatakiwa kuwa na vifaa hivyo ili kabla ya kumtibu mgonjwa aweze kujua yupo katika hali gani, pia kifaa hicho kina uwezo wa kubaini hali ya mtoto  ya lishe kwa kuangalia rangi ambazo zinaonyesha katika kifaa hicho ambapo ikiwa nyekundu huyo mtoto anakuwa katika hali ya hatari na ikiwa njano anakuwa salama.

Hayo yamesemwa na Afisa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Abel Gyunda wakati akitoa semina hiyo katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Afisa lishe amesema waganga wa tiba asili wanasaidia lakini tatizo la lishe haliwezi kutatuliwa na Mganga wa tiba asili ndio maana wameshirikishwa katika kikao hicho ili kupata elimu ya kuwatambua watoto wenye dalili za  utapiamlo mkali na kutoa  taarifa kwa mhudumu wa afya au mganga mfawidhi katika kituo kilicho karibu yake.

Ndg. Gyunda ameongeza kuwa katika Mkoa wa Simiyu kufikia mwaka jana takwimu za hali ya udumavu ilikuwa 32.1% ambapo katika watoto 100 watoto 32 wamepata udumavu, uzito pungufu ulikuwa 14.6% na ukondefu ulikuwa kwa 4.6% hiyo yote ni kwa sababu ya kutokupata lishe sahihi.

Afisa lishe amesema tatizo la lishe Duniani ni kubwa ili kukabiliana na tatizo hilo viongozi wana wajibu wa kuwaelimisha akina mama kutumia virutubisho vyenye madini chumvi, vitamin A na dawa za minyoo lengo la kurutubisha chakula ni kuondokana na matatizo makubwa ambayo yanasababishwa na ulaji wa vyakula duni hivyo vyakula vikirutubishwa vitasaidia akina mama kuepuka kujifungua watoto wenye matatizo kama  kuvimba kichwa.

Aidha, Ndg. Gyunda amewasisitiza watendaji wa Kata na waganga wa tiba asili endapo watambaini mtoto mwenye dalili za  udumavu, ukondefu wanatakiwa kutoa taarifa kwa wahudumu wa afya ili mtoto huyo aanzishiwe matibabu mara moja kwa kuwa tayari wamepewa vifaa maalumu ambavyo vitawasaidia kutambua mtoto kama ana dalili zozote za ugonjwa huo.

Afisa lishe ameendelea kusema katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kupitia mapato ya ndani  imetenga bajeti zaidi  ya  shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuwaelimisha waganga wa tiba asili, watendaji wa vijiji, watendaji wa kata na wahudumu wa afya katika masuala ya afua za lishe ili tatizo la utapiamlo kwa Wilaya ya Maswa liwe historia.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.