• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MRADI WA MAJI WENYE THAMANI YA SHS BILIONI 1.3 KUNUFAISHA WAKAZI 8361 WA KIJIJI CHA IPILILO

Posted on: April 9th, 2024

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Maswa imekagua mradi wa kisima chenye urefu wa mita 120 chenye uwezo wa kuzalisha maji lita 19,000 kwa saa sawa na lita 456,000 kwa siku ambapo ujenzi wa kisima hicho ukikamilika utaweza kuhudumia wananchi 8361 wa Kijiji cha Ipililo Kata ya Ipililo.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya ya Maswa ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amesema Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anataka wananchi wake wawe na furaha ikiwemo usalama, utulivu na amani pamoja na utoaji wa huduma za kijamii na za kiuchumi kwa wananchi.

Mhe Kaminyoge amesema hayo katika mkutano wa hadhara alioufanya katika Kijiji cha Ipililo wakati akizungumza na wananchi hao baada ya kamati ya usalama ya wilaya  kuhitimisha  ziara ya kukagua miradi   mbalimbali ya maendeleo.

“Mhe Rais alisikiliza maombi ya wananchi kupitia kwa viongozi mliowachagua mheshimiwa Diwani, Mhe  Mbunge ambaye ni mwakilishi wa wananchi kupeleka malalamiko yenu  kwa Mhe Rais, Mhe Rais amesikia na  ametoa kiasi cha shilingi bilioni 1.3  katika Kijiji cha Ipililo kwa ajili ya huduma ya maji.” amesema Mhe Kaminyoge

Pia amesema tayari kisima kirefu kimechimbwa na mkandarasi tayari yupo “site” akijenga jengo la miundombinu ya kuingiza umeme, pampu ili maji yaweze kuvutwa na kupelekwa kwenye tenki kwa ajili ya kupokea maji kutoka kwenye kisima ili kusambaza maji hayo sehemu mbalimbali za wananchi.

Mhe Mkuu wa Wilaya ameeleza kuwa mkataba wa mkandarasi ni wa  mwaka mmoja hivyo amemuomba kuharakisha mradi huo kwa kuwa mkandarasi huyo anafanya kazi kwa weredi mkubwa kwa kuwa tatizo la ukosefu wa maji kwa wananchi wa Ipililo ni kubwa na mkandarasi huyo ameahidi kufikia mwezi wa Tano mwaka huu wananchi watapata maji.

Ujenzi wa mradi huo unatekelezwa na wakala wa maji na Usafi wa Mazingira vijijini RUWASA.

Pia katika hatua nyingine Mhe Kaminyoge amesema  Mhe Rais ametoa kiasi cha shilingi milioni 79 kwa Kijiji cha Ikungulyankoma  na Kijiji cha Ipililo  shs milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa bweni la wasichana wanaotoka mbali  ili waweze kukaa shuleni na kuepukana na mimba zisizotarajiwa.  

Amesema mradi huo unatekelezwa kupitia miradi ya TASAF yenye masharti ya wananchi kuchangia nguvu kazi katika ujenzi huo ambapo tayari awamu ya kwanza ya ujenzi wa bweni  imefanyika katika shule ya Sekondari Budekwa na sasa mradi huo utafanyika katika shule ya Sekondari Ipililo hivyo amewataka wananchi kuchangia nguvu kazi ili ujenzi huo ukamilike kwa wakati.

Akizungumza kwa nyakati tofauti Mkuu wa Wilaya ametoa siku tatu kwa mkandarasi kuhakikisha anatengeneza Barabara zote ambazo ni korofi ili ziweze kupitika wananchi waweze kusafirisha mazao yao, ambapo  Barabara hizo ni Barabara ya Njiapanda- Muhida yenye gharama ya shs milioni  57 kutoka mfuko wa barabara.

Matengenezo ya Daraja la Wigelekelo Barabara ya Mwasayi- Masela yenye gharama ya Tsh milioni 325 ambapo mpaka sasa mradi huo umefikia asilimia 75%, mradi wa Barabara ya Bushashi – Ipililo wenye gharama ya Shs milioni 400 fedha hizo zimetoka mfuko wa tozo za mafuta.

"Sisi tunaopewa hela na serikali kwa ajili ya kutengeneza miundombinu na huduma mbalimbali za wananchi tusiwe kikwazo kwa wao kupata huduma nzuri, hizi Barabara sio za TARURA ni za wananchi wa Maswa kwa usimamizi wa Mkuu wa Wilaya." Amesema mkuu wa wilaya.

Pia amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa makalavati yote kwa muda wa wiki moja katika Barabara hizo.

Pia kamati ya usalama ya Wilaya imekagua  ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa lililopo Ng'hami Kata ya Nyalikungu pamoja na ujenzi wa tanki la maji Mwashegeshi mradi unaosimamiwa na MAUWASA.

Jengo la Utawala la Halmshauri

Tank la Maji Mwashegeshi



Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.