• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mfumo wa stakabadhi ghalani watambulishwa kwa Madiwani

Posted on: November 17th, 2023

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu wamepata elimu ya mfumo wa stakabadhi ghalani yenye lengo la kuwajengea uwezo Madiwani na wataalamu kuhusu matumizi ya mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuwaelimisha wakulima katika kuuza mazao   ili wakulima wawe na   uhakika wa kuuza mazao kwa bei wanayoitaka.

Hayo yamesemwa na Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Simiyu Bw. Godfrey Mpepo katika kikao cha Baraza la madiwani cha robo ya kwanza ya mwaka wa Fedha 2023/2024  kilichofanyika tarehe 16.11.2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambapo madiwani walikuwa wakiwasilisha taarifa za Kata zao.

Alisema. Mfumo wa stakabadhi ghalani ni hati iliyopo kwenye karatasi au mfumo wa mtandao ambayo inatolewa kwa mwenye mali ambaye ni mkulima baada ya kupeleka mazao yake kwenye ghala husika ambalo linakuwa limepewa leseni na Mamlaka ya maghala nchini.

"Mfumo wa stakabadhi ghalani unahamasisha sana  na unakusudia sana kupokea mazao ghalani yale yenye ubora, na huo ubora unathibitishwa kwa vipimo kila zao linapimwa kwa vifaa vyake hata likipelekwa nje ya nchi linaitangaza Tanzania aidha hizi dengu, choroko au pamba zimetoka Tanzania zikiwa na ubora wa kimataifa." Amesema Mpepo

Aidha Mpepo amesema dhumuni kubwa la stakabadhi ghalani ni kurasimisha mifumo ya masoko kwa lengo la kupinga vipingamizi mbalimbali vinavyosabanisha kukwamisha uzalishaji wenye tija na utafutaji wa masoko wa mazao yanayozalishwa.

"Uzuri wa stakabadhi ghalani unapata mazao yenye ubora kabisa kwa maana kwamba mazao yanakuwa bora ili yaweze kuingia sokoni ni lazima yathibitishwe na vipimo vya ubora wa soko au wa zao husika kwa maana kwamba mazao mengi nchini kwetu yanakuwa yamenunuliwa kwenda kutumiwa nje ya nchi ili yaweze kwenda nje kimataifa yanatakiwa kuthibitishwa". Amesema Mrajisi Msaidizi wa vyama vya Ushirika

Kaimu Mrajisi wa vyama vyaushirika amesema taarifa za mkulima zikiwepo mtandaoni zitamsaidia katika masoko kuongeza bei katika mazao pamoja na kuondoa uhaba wa mitaji kwa sababu mkulima akizalisha taarifa zake zitapatikana mtandaoni hivyo kumfanya aweze kupata mkopo benki.

Mfumo huo pia utasaidia wanunuzi wengi kununua mazao mbalimbali ambayo yataliongezea Taifa Fedha za kigeni ambazo zitachangia kuongeza mapato kwa upande wa serikali kutokana na wanunuzi kutoka nchi mbalimbali wataweza kununua mazao hayo kwa njia ya mtandao.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mpindo  Mhe. Amos Ntambo amewashukuru wataalamu kwa kuja na wazo hilo la kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuwa ni mfumo mzuri ambao utawasaidia wakulima kupata bei nzuri na kuzisaidia Halmashauri za Mkoa wa Simiyu kuongeza mapato na pia madiwani wameomba elimu itolewe zaidi ili wawe na uelewa zaidi.

Stakabadhi ghalani inahusisha masoko level ya mtandao yaani unaweza ukauza bidhaa kupitia mtandao, na tayari Mikoa ya Mtwara, lindi na Songwe wanatumia mfumo huo wa stakabadhi ghalani ambao umewasaidia wakulima kupanga bei za mazao katika soko kwa sababu taarifa zote za bei zinakuwa mtandaoni.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.