• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Madiwani wapata mafunzo ya matumizi ya vishikwambi

Posted on: October 17th, 2022

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wamepata mafunzo ya matumizi ya vishikwambi  kwa ajili  ya shughuli mbalimbali za maendeleo katika Kata zao ikiwemo taarifa za kata ambazo zitasomwa katika robo ya kwanza ya mwaka 2022/2023.

Akitoa semina hiyo katika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Afisa TEHAMA Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Edwin Bairu amewasisitiza waheshimiwa Madiwani kuwa, Baraza na Kamati zote zitatumia teknolojia ya kidigitali katika kuendesha shughuli zote za vikao kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa tayari imenunua  vishikwambi vitakavyotumika kwa matumizi ya vikao hivyo ambavyo tayari vimewekewa programu maalumu ambayo taarifa zote zitatumwa humo.

Aidha Afisa TEHAMA amewasihi waheshimiwa Madiwani kutumia wenyewe  vishikwambi na si vinginevyo ili kuepusha uharibifu utakaojitokeza ikiwepo kuvunjika au kupotea na kuweka taarifa katika usalama.  Pia amewaomba waheshimiwa Madiwani kufanya mazoezi ya mara kwa mara ili wapate uzoefu haraka wa kutumia vishikwambi hivyo.

Akizungumza katika semina hiyo Afisa manunuzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa amewasihi waheshimiwa Madiwani kuvitunza vishikwambi hivyo kwa kuwa ni Mali ya serikali pamoja na kuvitumia kwa matumizi ya serikali tu na si vinginevyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa amewaomba waheshimiwa Madiwani kufanya kazi kwa karibu na watendaji wa Kata zao katika kuandaa taarifa zao na usimamiaji wa miradi maendeleo. Pia amewasisitiza waheshimiwa Madiwani ambao hawajapata vishikwambi wawe na subira kwa kuwa bajeti iliyowekwa imetosha vishikwambi vya Madiwani wa kata 36 tu  ambavyo vitasaidia utendaji kazi wa waheshimiwa Madiwani na kupunguza gharama za uendeshaji wa vikao na kuongeza ufanisi.

Kwa upande wao waheshimiwa Madiwani wamefurahi kupata elimu hiyo na kuiomba Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kuona utaratibu wa kufanya ili Madiwani wa viti maalum nao waweze kupata fursa ya kupata vishikwambi ili kuleta chachu ya uwajibikaji.



Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.