Kikao cha Baraza la Madiwani Wilayani Maswa cha kujadili rasimu ya mpango na bajeti ya mwaka 2019/2020 limefanyika tarehe 20-21/2/2019 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.
Mjadadala umefanyika kwa weledi mkubwa na hatimaye kuweza kupitisha rasimu yenye kiasi cha shilingi 43,805,316,556.34 itakayotumika katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali ikiwemo miradi ya maendeleo.
Kupitia mjadala huo, Wah. Madiwani wamelalamikia mchezo wa bonanza Wilayani Maswa. Wamesema unaharibu watoto wao maana mienendo yao imeanza kuwa mibaya inayopelekea kuuza vyakula, vifaa vya nyumbani na upotevu wa muda wa kufanya shughuli za maendeleo. Sambamba na hili wamedai mwisho wa michezo hii inaweza kutengeneza kizazi chenye matatizo ikiwa ni pamoja na wezi, vibaka na watu wasiojisimamia.
Pia michezo hii imeweza kusababisha matatizo katika familia nyingi hasa kwa baadhi ya Wazazi kuchukua mapato ya familia na kuyatumia katika mchezo huo. Wazazi hao wengine wametumia mda wao vibaya kwa kupotezea kwenye mchezo huu na hata wakati mwingine kurudi muda umeenda sana.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.