• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Maafisa Ugani Maswa wapata mafunzo ya kilimo bora cha Karanga

Posted on: November 6th, 2023

Maafisa Ugani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu wamepata mafunzo ya kanuni bora za kilimo cha zao la Karanga yenye lengo la kuwajengea uwezo wa namna ya kukabiliana na magonjwa mbalimbali, nafasi ya  upandaji na matumizi ya mbegu bora za Karanga.

Mafunzo hayo yametolewa na wataalamu kutoka Taasisi ya Kilimo Tanzania TARI leo tarehe 6.11.2023 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambapo maafisa ugani zaidi ya 20 wamehudhuria kwa ajili ya kupata mafunzo hayo ili wakawawezeshe wakulima kulima kilimo bora ambacho kitawasaidia  kuvuna mavuno kwa tija.

Akitoa elimu hiyo mratibu wa program ya utafiti wa zao la Karanga nchini  Dr Happy Daudi kutoka kituo cha Naliendele amesema wamefika katika Halmashauri ya Wilaya ya  Maswa kwa ajili ya kuwajengea uwezo maafisa ugani wote kuhusu kilimo bora cha zao la  Karanga kwa  kuwa wao ndio wanaoweza kutatua changamoto mbalimbali za wakulima.

Ameongeza kuwa katika kilimo cha Karanga wakulima wengi hawatumii mbegu bora za Karanga hivyo kupitia mafunzo hayo Dr Happy ametoa wito kwa maafisa ugani kuanzisha vikundi vya kuzalisha Karanga ili kupata mbegu bora ambazo zimethibitishwa kitaalamu na taasisi za utafiti wa kilimo.

Pia amesema  kutokana na mafanikio  waliyoyapata  wakulima ambao walilima mbegu aina ya Mangaka 2009  taasisi hiyo imetoa kilo 100 za mbegu hiyo ya Mangaka 2009 kwa kuwa ni mbegu nzuri inayofaa kwa ardhi ya Maswa ambapo katika eneo la nusu heka wakulima  wamepata gunia 16,  ili kutanua kilimo chao maafisa ugani wana jukumu la  kuwajengea uwezo wakulima kutumia mbegu bora na kufuata kanuni za kilimo bora cha Karanga.

Nae Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Masalu Shibiliti ameishukuru taasisi ya  utafiti wa kilimo TARI Naliendele kwa kutoa mafunzo hayo kwa Maafisa Ugani ambayo yatawasaidia wakulima kulima kilimo ambacho kitazingatia mbegu bora kwa kuwa wakulima wengi wa Wilaya ya Maswa hawatumii mbegu bora za Karanga hivyo ujio wa mbegu hizo utaongeza tija katika uzalishaji wa zao hilo.

Ameongeza kuwa wakulima wa Maswa watanufaika kutokana na elimu hiyo kwa kuwa maafisa ugani wataweza kuwaelimisha namna ya kupanda kwa kuzingatia kanuni za upandaji wa sentimeta 10 kati ya mmea na sentimeta 50 kati ya mstari, udhibiti wa sumu kuvu na magonjwa mbalimbali katika zao hilo lengo likiwa ni kumfanya mkulima kupata matokeo.

Aidha mafunzo hayo yatawasaidia maafisa ugani kuwaelimisha wananchi kutumia mbegu bora za zao la Karanga sambambamba na hilo Halmashauri itaunga mkono jitihada hizo kwa kuweka kipaumbele cha zao hilo katika maonyesho ya  wakulima nanenane ili wakulima wengi wapate elimu hiyo na kuanzisha mashamba darasa kila Kata ambapo mpaka sasa tayari Kata 3 zimeanza uzalishaji.

Kwa upande wake Afisa Ugani wa Kata ya Isanga Fred Fidelis amesema katika Kata yake wakulima walikuwa wanalima mbegu zisizo za kisasa hivyo kupitia mafunzo hayo wanaishukuru taasisi hiyo ya Naliendele kwa kuwapatia mbegu za kisasa ambazo zitawasaidia wakulima.

Nae Bibi shamba wa Kata ya Nyalikungu Elin Nashoni amewashukuru wataalamu kwa mafunzo hayo ambayo yamekuja kwa muda sahihi ambapo wakulima watapata elimu ya namna bora ya kulima kwa  nafasi ya upandaji wa mbegu hizo hivyo kupitia wataalamu tayari Wilaya ya Maswa imeanzisha vikundi ambavyo vitazalisha mbegu ambazo baada ya miaka miwili Maswa itapata mbegu bora za karanga  ambazo zitatumika kwa ajili ya uzalishaji.

Godson Makoye Afisa kilimo Kata ya Sukuma anaishukuru serikali kupitia taasisi ya utafiti wa kilimo TARI Naliendele kwa mafunzo waliyoyatoa ambayo yamewasaidia kujua aina mbalimbali za Karanga na kulima bila kuchanganya na zao lingine hivyo ameahidi kupitia mafunzo hayo atawaelekeza wakulima kupitia mashamba darasa kulima kwa tija ili wapate magunia 20 na kuendelea kwa heka tofauti na sasa ambapo wanapata magunia 2 mpaka 3.

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.