• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kongamano la maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru lafana Maswa

Posted on: December 9th, 2022

Maadhimisho ya miaka 61 ya uhuru yamefanyika wilayani Maswa kwa kongamano lililohusisha wadau mbalimbali kujadili maendeleo endelevu yaliyofanyika wilaya ya Maswa kwa kuangazia sekta mbalimbali  za wilaya  ya Maswa

Akizungumza katika kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Maswa mkuu wa wilaya Mhe Aswege Kaminyoge amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kuelekeza fedha hizo zilizotengwa kwa ajili ya sherehe za uhuru kwenda kujenga shule 8 za watoto wenye mahitaji maalumu

Pia mkuu wa wilaya amewapongeza wadau mbalimbali kwa kufika katika kongamano hilo ili waweze kupata mwanga namna ambavyo serikali imepiga hatua toka kipindi cha Uhuru mpaka sasa miaka 61na kwenda kuwaeleza wananchi maendeleo ambayo yamefanyika tangu uhuru mpaka leo.

Wakitoa taarifa kwa wadau hao sekta mbalimbali zimeeleza mafanikio ambayo yamepatikana tangu uhuru mpaka sasa serikali imepiga hatua kubwa sana kwenye miradi ya maendeleo katika wilaya hii ya Maswa

Sekta ya Maji

Maji ni uhai kauli hii inakuja ikiwa nchi ya Tanzania inaadhimisha miaka 61 ya uhuru kutoka kwa wakoloni tatizo la maji limesababisha ndoa nyingi kuvunjika, watu kutembea umbali mrefu kutafuta maji lakini serikali kupitia wizara ya maji  ililiona hilo na kuja na mwarobaini wa tatizo hilo kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya maji mijini na vijijini.

Katika wilaya ya Maswa tatizo la maji katika miaka ya  arobaini lilikuwa kubwa sana na kupelekea wananchi kuhangaika sana kwa kuwa kulikuwa na kisima kimoja tu hapa mjini kilichokuwa mlima wa Nyalikungu, baadaye  bwawa la Zanzui lilitengenezwa lakini halikuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wote.

Akitoa taarifa  ya mafanikio katika sekta ya maji mwakilishi wa Mkurugenzi wa MAUWASA amesema katika wilaya ya Maswa hapakuwa na Maji ya uhakika  kabla ya uhuru lakini baada ya uhuru Viongozi mbalimbali walifanya juhudi kubwa ambazo zilileta matokeo na kuweza kupatikana chanzo Cha kudumu Cha bwawa la Zanzui maarufu “New Sola” ambalo linahudumia mji wote wa Maswa, mtandao wa mabomba umeongezeka na kuwa kichochea Cha maendeleo  katika wilaya ya Maswa bwawa hilo linahudumia takribani wananchi wote wa Maswa mafanikio makubwa ambayo serikali imeyafanya na inaendelea kuyafanya katika mji wa Maswa na vijiji vya Maswa kwa kuwa Sasa maji yanapatikana kwa asilimia 78.4 mjini

Kwa upande  wa vijijini maji yanapatikana kwa asilimia 74.5,  visima vifupi 1500 vimejengwa ambavyo vinatumia pampu za mkono, visima virefu 12 ambavyo vinatumia huduma ya mtandao wa Bomba, pia serikali imefanya jitihada kubwa kwa kuweka mtambo wa kutibu na kusafisha maji katika bwawa hilo ambalo limepunguza magojwa ya mlipuko.

Aidha serikali imeendelea kuongeza miundombinu ya maji ambapo kuna mradi wa bonde la ziwa Victoria ambao utasaidia wananchi wa vijiji vya  Sen'gwa, Mwabomba na maeneo mengine ya mji wa Maswa, pia  miradi mingine 4 ya UVICO Sulu kwenda Inenwa mpaka Kizungu  na maeneo jirani.

Sekta ya Elimu

Hii ni sekta ambayo imeboreshwa kwa kiasi kikubwa kwa kuwa Elimu kabla ya uhuru ilitolewa ili kusaidia wakoloni katika shughuli zao lakini baada ya uhuru serikali ilikuja na azimio la Arusha ambalo lililenga kutoa Elimu ya kujitegemea na ujamaa, tangu mwaka 1961 kulikuwa na Shule 39 tu za sekondari nchi mzima

Kwa upande wa wilaya ya Maswa haikuwa na Shule ya sekondari wakati huo wa uhuru lakini serikali za awamu zote ziliweka juhudi ya kujenga shule mpaka kufikia sasa Maswa ina jumla ya Shule za Sekondari 45 zenye wanafunzi zaidi ya 7000 na vyumba vya madarasa 352 kutoka ziro mwaka 1961

Hii imechangia kwa kiasi kikubwa miradi mingi ya Elimu kukamilika na kuongeza ufaulu wa wanafunzi kwa kuwa hali ya ufaulu imefikia asilimia 97 kwa upande wa kidato Cha nne na asilimia 100 kidato cha Sita. Kwa upande wa Sekondari hayo ni mafanikio makubwa sana yaliyofanywa na serikali mpaka sasa miaka 61 ya uhuru na Shilingi bilioni 3.9 zimetolewa katika sekta ya Elimu kwa ajili uwekezaji mwaka 2021 mpaka sasa .

Sekta ya umeme

Maendeleo hayawezi kupatikana pasipo kuwepo kwa nishati ya umeme katika kipindi Cha miaka ya 1961 wilaya ya Maswa haikuwa na umeme lakini serikali imewekeza fedha nyingi ili kuhakikisha wananchi wa Maswa wanapata umeme na leo Tanzania inaadhimisha miaka 61 ya uhuru katika wilaya ya Maswa kwa kuwa na mafanikio makubwa.

Akiwasilisha taarifa hiyo mwakilishi wa meneja wa TANESCO wilaya ya Maswa Ndg Ali Nkuba amesema umeme ulifika Maswa mwaka 1992 na ilikuwa ni eneo la hapa mjini tu lakini maendeleo yamefanywa na serikali kwa kuwa mpaka sasa vijiji vyote 120 vya Maswa vimepata umeme na serikali inaendelea kusambaza umeme mpaka kwenye kila Kitongoji ili kumwezesha kila mwananchi aweze kunufaika na huduma hiyo ambayo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Serikali.

Pia Nkuba amewahakikishia wananchi wa Maswa kuwa tatizo la umeme litapungua kwa kiasi kikubwa kwa kuwa tayari kuna mradi mkubwa wa kujenga kituo Cha kupozea umeme kitajengwa Kijiji Cha Imalilo wilaya ya bariadi.

Sekta ya afya

Huduma ya afya ilianza rasmi mwaka 1959 katika Kijiji cha Malya Magereza , Mpindo 1960 na jengo la magreth kama zahanati na baadae kuwa hospitali ya wilaya hivyo kabla ya uhuru kulikuwa na hospitali tatu.

Baada ya uhuru

Huduma za afya zimeendelea kuongezeka ambapo mpaka sasa kuna vituo 54 vya Serikali vinavyofanya kazi katika maeneo mbalimbali, Hospitali ya Wilaya 1, Vituo vya Afya 4 na Zahanati 49, Vituo 2 kutoka mashirika ya dini na Zahanati 2 vya Magereza ya Maswa na Malya pamoja na Zahanati 2 za watu binafsi.

Akiwasilisha taarifa hiyo katika kongamano hilo Mganga Mkuu wa Wilaya amesema huduma za afya zimefika  vijiji 51 ambavyo kuna Zahanati na Vituo vya Afya na vingine vinaendelea kijengwa mpaka kufikia mwaka huu kutakuwa na zahanati na vituo vya afya 64 vinavyotoa huduma hiyo, hayo ni mafanikio makubwa ambayo serikali imeyafanya katika Wilaya ya Maswa .

Pia kwa kujengwa kwa vituo hivyo vinne vya afya ambavyo vina uwezo wa kufanya upasuaji itapunguza vifo vitokanavyo na uzazi hasahasa mama mjamzito badala ya kusafiri umbali mrefu sasa ataweza kupata huduma hiyo hukohuko kwenye kituo Cha karibu yake.

Mganga Mkuu amebainisha kuwa Hospitali imeimarisha huduma za dawa kwa kuwa dawa muhimu zote zinapatikana kwa asilimia 97 na pia majengo yameendelea kuboreshwa kwa kujenga jengo la dharura ambalo litaokoa maisha ya wanachi wengi wa Wilaya ya Maswa.

Kwa upande wao wadau mbalimbali wameipongeza serikali kwa kuendelea kuleta maendeleo katika Wilaya ya Maswa na kuomba amani na upendo iendelee kudumu, pia wameomba watendaji waendelee kukemea tabia ya ukatili wa kijinsia na kuwashirikisha wadau kwenye vikao mbalimbali nao waweze kuchangia mawazo ya kuipeleka mbele Wilaya ya Maswa katika maendeleo .

Pia wameiomba Serikali kuongeza vyuo vya VETA ambavyo vitasaidia watoto waliomaliza shule  waweze kupata mafunzo ambayo yatawasaidia kujiajili wenyewe, wataalamu kusimamia kwa karibu miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ili idumu zaidi pamoja na ukarabati wa Barabara ambazo hazipitiki ikiwepo ya Malampaka mpaka Mwigumbi.

Maadhimisho hayo yamehitimishwa kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa wanamichezo ambao walishinda katika uandishi wa insha na mpira wa miguu na kuwasisitiza wananchi wote kutangaza maendeleo yaliyofikiwa miaka 61 ya uhuru.

"Amani naupendo ndio nguzo ya maendeleo yetu"

Mgeni rasmi Mhe. Aswege Kaminyoge Mkuu wa Wilaya ya Maswa akifungua kongamano la maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru 9/12/2022

Wadau mbalimbali waliohudhuria kongamano la miaka 61 ya Uhuru katika Ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa 9/12/2022

Mgeni rasmi akimpongeza Mwanafunzi  wa Shule ya Msingi Nyalikungu aliyeshinda Insha kuhusu mafanikio ya miaka 61 ya Uhuru

Katibu Tawala Wilaya ya Maswa akitoa neno la Shukrani kwa wote waliohudhuria kongamano 9/12/2022



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.