• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kikao kazi Cha SIPSEA chafanyika Maswa

Posted on: May 5th, 2023

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu Mkoa wa Simiyu Ndg John M. Tilubuzya  amewataka waandishi waendesha ofisi kutembea kifua mbele kwa kujiamini, kwa sababu  serikali inatambua umuhimu wao katika utendaji kazi.

Akizungumza wakati akifungua kikao hicho cha waandishi waendesha ofisi (PS) kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa leo tarehe 05. 05.2023 na kuudhuriwa na waandishi waendesha ofisi 40 kati ya 67 kutoka katika Wilaya zote za Mkoa wa Simiyu.

“Katika utumishi wa umma kada yenu ni kada muhimu sana na kutokana na umuhimu huo ndio maana hata Mhe.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan ameona ni bora kukutana na nyie, Ukipata mwaliko wa Mhe. Rais wewe ujue wazi kabisa una umuhimu mkubwa katika uendeshaji wa shughuli za serikali”. Amesema Tilubuzya

Ndg Tilubuzya amewapongeza SIPSEA   kwa ushirikiano ambao wameuonyesha kwa kuanzisha chama  chao ambacho wamekisajili ili kiwasaidie kwenye mambo mbalimbali katika kutatua changamoto walizonazo ikiwemo misiba na sherehe.

Katibu tawala msaidizi sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu ametoa wito kwa wanachama wote kushirikiana katika  kutoa michango kila mwezi kama ilivyo ada na wale wote walio katika kada hiyo ambao  hawajajiunga katika chama  hicho watoe  michango ambayo itasaidia mwanachama yeyote atakayepata shida kusaidiwa kwa urahisi ili kudumisha umoja huo.

Ndg Tilubuzya hajaridhishwa na maudhurio ya waandishi waendesha ofisi hao ambapo amewaahidi ataongea na wakurugenzi wa wilaya ili kuwaeleza picha harisi kwa kuwa hata nusu yao hawakufika na kujua sababu zilizosababisha watumishi hao wasihudhurie kikao hicho.

Awali akitoa taarifa kwa mgeni rasmi  Katibu wa Umoja wa Waandishi  Waendesha Ofisi Mkoa wa Simiyu (SIPSEA) Loyceah J Ishengoma amesema umoja huo ulianza 29 Aprili,  2019 ukiwa na wanachama 32 ambapo mpaka sasa wapo wanachama 67

Ishengoma amesema lengo la kuanzisha chama hicho  katika Mkoa wa Simiyu ni kuwaunganisha pamoja waandishi waendesha ofisi, kuwa na umoja imara, kusaidiana kwenye shida na raha ikiwemo misiba na sherehe.

Aidha amesema kuwa kutokana na changamoto wanazokutana nazo wameomba kupatiwa mafunzo ambayo yatawajengea uwezo kwa kuwezeshwa fedha, kupewa vibari na waajiri wa taasisi mbalimbali kwa ajili ya mafunzo ya kitaaluma ndani na nje ya Mkoa.

Kikao hicho kinafanyika ikiwa ni ratiba ya chama hicho kukutana kila mwaka kujadili mambo mbalimbali yaliyotekelezwa kwa mwaka uliopita, kupata taarifa ya mapato na matumizi pamoja na kutatua changamoto ambazo hazijapatiwa ufumbuzi katika maeneo ya kazi.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.