• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kikao cha Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, wadau wa Elimu Wilayani Maswa

Posted on: January 19th, 2018

Leo tarehe 19/1/2018 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Ndg. Jumanne A. Sagini amefanya kikao maalumu na wadau wa elimu katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kilicholenga suala zima la kusimamia taaluma ili kuinua kiwango cha elimu.

Kikao kimejumuisha Wakuu wa Idara, Maafisa Elimu Wilayani na Kata, Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu Wilayani Maswa. Kiongozi huyu amewataka wakuu wa Idara na Vitengo kuwa na ushirikiano wa pamoja katika kusimamia suala zima la elimu Wilayani Maswa ili kuinua kiwango cha ufaulu.

Amesema “pamoja na wingi wa wanafunzi, uchache wa walimu, mwitikio hafifu wa Wazazi katika suala la elimu hapa Wilayani, changamoto hizi zote na nyinginezo zisitufanye tubweteke bali tunatakiwa kujipanga kusimamia suala zima la elimu kwa kutumia taaluma tulizonazo”. Amesisitiza walimu wasimamie taaluma na siyo kazi nyingine.

Amewataka Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu wawachukulie hatua / wawajibishe Walimu walevi, watoro na wasiofundisha ipasavyo kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni za kazi. Ameongeza kwa kusisitiza kuwa Watumishi walevi, watoro kazini na wasiotimiza wajibu wao siyo rahisi kupandishwa daraja / cheo pamoja na watumishi wanaowajibika.

Aidha Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu amewaagiza Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu wasio na kipindi hata kimoja cha kufundisha kwa wiki kuanzia sasa wawajibike pia kufundisha. Ameenda mbali kwa kuwataka Maafisa Elimu Kata pia wapate muda wa kwenda kufundisha.

Kwa kupiti kikao hiki Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu Ndg. Julius Nestory ametoa maagizo yafuatayo:

  1. Kila Afisa Elimu Kata au Mkuu wa Shule au Mwalimu Mkuu asiyekaa katika eneo lake la kazi wamepewa siku saba (7) kuanzia leo wawe wamehamia katika maeneo ya vituo vyao vya kazi.
  2. Wakuu wa shule, Walimu wakuu na walimu wote kwa ujumla wasifike Ofisi za Mkurugenzi au Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufikisha taarifa bali wawakabidhi Maafisa Elimu Kata kufikisha taarifa hizo kwani wao wana nyenzo au usafiri wa kuwafikisha katika vituo hivyo na kurejesha taarifa hizo.

Katika kuhitimisha Katibu Tawala Wilaya ya Maswa Ndg. Rutalemwa P. Rutagumirwa amesema kila Mwalimu atimize wajibu wake ili kuweza kuinua kiwango cha elimu Wilayani Maswa. Amesisitiza kwa kauli mbiu hii “Kwa pamoja tuseme tutabadilika na tutaleta mageuzi ya Elimu, hivyo ufaulu utaongezeka Wilayani Maswa”


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.