Kampeni ya kutokomeza mimba na ndoa za utotoni ilianzishwa na mkuu wa Wilaya ya Maswa imeanza utekelezaji katika Tarafa ya Sengerema Wilayani Maswa ambapo mkuu wa wilaya amekutana na Wazazi, Walezi, Walimu na Wanafunzi katika shule ya Sekondari Shishiyu na kujadiliana mambo ya utekelezaji ili kufanikisha kampeni aliyoianzisha. Katika kampeni ameambata na Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya,Mkurugenzi Mtendaji na Kamati ya kutokomeza mimba na ndoa za utotoni ya Wilaya.
Ametumia fursa hiyo kuwaomba wazazi hao kuwekeza katika elimu kwa watoto wao ili kuleta maendeleo katika jamii inayowazunguka. Aidha amesema ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni katika jamii yetu wazazi wanatakiwa kusimamia malezi bora ya watoto wao kwani malezi mazuri huanzia kwenye familia na si vinginavyo. Hivyo kila mzazi au mlezi anatakiwa kutekeleza hilo ili kufanikisha kauli mbiu isemayo " Tokomeza mimba na ndoa za utotoni, tokomeza mimba mashuleni, elimu mpaka chuo kikuu inawezekana".
Kwa upande wa wanafunzi amewahasa kuanza kuweka malengo ya nani anataka awe hapo baadaye ili pindi anaposoma alenge pale anapopataka au anapopakusudia, "Kuweni na ndoto kuanzia sasa za nani unataka uwe baada ya shule".
Wadau wote wameunga mkono kampeni hii kwa kuchangia mawazo mbalimbali; Mzazi mmoja amewataka Wazazi waongeze ushirikiano zaidi wa kuwasimamia watoto wao hasa kwa kuwapa mahitaji mhimu na kuelewa nyendo zao.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.