• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI YA FEDHA UTAWALA NA MIPANGO YARIDHISHWA NA USIMAMIZI WA MRADI YA MAENDELEO WILAYA YA MASWA

Posted on: November 7th, 2024

Kamati ya Fedha Utawala na Mipango ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe Paul Maige imewapongeza viongozi wanaosimamia miradi katika Wilaya ya Maswa kwa usimamizi mzuri wa mradi unaotekelezwa katika maeneo yao.

Wajumbe wa kamati hiyo wametoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti wakati walipofanya ziara kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo, ambapo wakiwa katika Hospitali ya Wilaya wamekagua mradi wa ujenzi wa majengo mbalimbali ikiwemo jengo la mionzi, jengo la maabara, jengo la kichomea taka na jengo la wodi ya gredi katika Hospitali hiyo iliyopo katika Kata ya Sola tarehe 06 Novemba 2024.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nyabubinza Mhe Emmanuel Ndalahwa amemshukuru Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali katika Wilaya ya Maswa ikiwemo mradi wa majengo mbalimbali  katika Hospitali ya Wilaya.

Pia mjumbe huyo alitaka kufahamu kama mradi huo utakamilika kwa muda uliopangwa, akijibu swali la mjumbe huyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dr Hadija Zeggega amesema mradi huo utakamirika kwa wakati kwa kuwa mkandarasi yupo katika hatua za ukamilishaji na kuweka milango katika jengo la mionzi.

Mjumbe wa kamati hiyo Diwani wa Kata ya Jija Mhe. Walwa Lubinza amewapongeza viongozi wa Hospitali kwa kuwa kazi imefanyika kwa kiwango kikubwa katika majengo yote pamoja na kusimamia vizuri fedha za miradi.

Pia mjumbe wa Kamati hiyo ambaye ni  Diwani wa Kata ya Mbaragane Mhe. Abel Masunga   amewataka viongozi hao kuendelea kuwa na moyo wa kusimamia fedha za serikali zinapotolewa ili kuhakikisha zinakamilisha mradi kwa muda muafaka.

Akisoma taarifa hiyo kwa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Maswa Dr Deogratias Mtaki amesema Wilaya ya Maswa ilipokea fedha kiasi cha shilingi milioni 900 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umeme katika Hospitali ya Wilaya.

Pia amesema mradi huo unatekelezwa na mkandarasi aliyepatikana kupitia mfumo wa NEST ambapo mradi huo ulianza tarehe 14 Februari 2024 na ulitarajiwa kukamilika 12 oktoba 2024 lakini mkandarasi aliomba kuongezewa muda na sasa mradi huo  atakabidhi 15 Novemba 2024.

Pia amefafanua matumizi ya fedha hizo ambapo amesema jengo la miozi litagharimu zaidi ya milioni 256, jengo la maabrara lina thamani ya zaidi ya shilingi milioni 322, jengo la wodi ya gredi lina thamani ya zaidi ya shs 231 na jengo la kichomea taka lina thamani ya zaidi ya shs milioni 41.

Aidha mganga mfawidhi amesema wilaya imeendelea na ukarabati wa miundombinu ya umeme yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 47 katika majengo 6 ambayo ni wodi ya watoto, RCH, wodi ya wazazi, bima, stoo ya dawa pamoja na power house block ambapo mpaka sasa fedha zilizotumika ni shilingi milioni 408.9 na kiasi kilichobaki ni shilingi milioni 419.

Aidha Dr Mtaki amesema mradi huo utakapokamilika utasogeza huduma kwa wananchi, kuongeza wigo wa matumizi ya Teknolojia na ufungaji wa mitambo ya kisasa ya maabara  na mashine ya mionzi itawapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali wa kilometa 53 waliokuwa wanatumia kwenda Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa Simiyu.

Pia wajumbe wa kamati hiyo wamekagua mradi wa ujenzi wa  jengo la Utawala, mradi wa ujenzi wa nyumba ya Mtumishi ( 2 in 1) katika Zahanati ya Mwang’anda iliyopo Kata ya Kadoto  pamoja na mradi wa ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu 6 ya vyoo katika shule ya msingi Mwawayi iliyopo Kata ya Nyalikungu.

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ikikagua ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa tarehe 06 Novemba 2024

Muonekano wa Jengo jipya la Maabara katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa

Muonekano wa Jengo jipya la Wodi ya gredi katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa

Muonekano wa Jengo jipya la kichomea taka katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa

Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mwawayi akitoa maelezo kwa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wakati ilipotembelea na kukagua ujenzi wa Vyumba vinne vya Madarasa na Matundu sita ya choo tarehe 06 Novemba 2024

Mganga Mkuu  wa Wilaya ya Maswa akitoa maelezo kwa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wakati ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa majengo ya Maabara, Mionzi, Wodi ya gredi na kichomea taka tarehe 06 Novemba 2024






Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.