Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango (FUM) imefanya ziara katika miradi mitatu ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kuona utekelezaji unavyoendelea kufanyika na kuwaomba wataalamu kusimamia miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa muda uliopangwa
Wakiwa katika ziara hiyo iliyofanyika Leo tarehe 25.10.2022 kamati imeridhishwa na ujenzi wa miradi hiyo inayotekelezwa katika maeneo hayo ambayo ni Mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Mashimba iliyopo Kata ya Badi ambayo ujenzi wake upo katika hatua nzuri na Mwezi Januari mwakani wanafunzi wanatakiwa kusoma katika shule hiyo, Mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari katika Kata ya Nyalikungu ambapo mradi huo ukikamilika utahudumia watoto wa eneo hilo ambao utapunguza changamoto ya watoto kutembea mwendo mrefu kutafuta shule.
Mradi wa ujenzi wa kituo Cha afya awamu ya pili katika Kata ya Badi ambapo mradi huo upo katika hatua ya msingi na ukikamilika utasaidia wananchi wa eneo hilo katika huduma za afya ili kupunguza vifo katika jamii ya eneo hilo.
Kwa upande wao wajumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wameipongeza serikali kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya miradi ambayo inaendelea maeneo mbalimbali ya Maswa na kuwaomba viongozi wanaosimamia miradi hiyo kuwa karibu zaidi ili Miradi hiyo ikamilike kwa wakati.
Nao wataalamu wameahidi kusimamia kwa karibu miradi hiyo na changamoto zote ambazo zimejitokeza zitatatuliwa kwa wakati ili wananchi pamoja na wanafunzi waweze kutumia miundombinu hiyo pia ushauri wa kamati wameupokea na wameahidi kuutendea kazi kwa nguvu zote.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.