• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DED MAISHA AHAIDI PIKIPIKI 2 KWA MWALIMU MKUU NA MWALIMU ATAKAYEFAULISHA KWA WASTANI WA "A" KATIKA MTIHANI WA DARASA LA SABA

Posted on: August 7th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Maisha Mtipa ameahidi zawadi ya pikipiki mbili kwa Mwalimu Mkuu na Mwalimu atakayefaulisha mtihani wa darasa la saba mwaka 2024 kwa wastani "A"

Ndg. Mtipa aliyasema hayo katika kikao cha cha kutathimini matokeo ya mtihani wa Mock kanda ya ziwa kilicchowashirikisha umoja wa wakuu wa shule za msingi Wilaya ya Maswa ambacho kilifanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Lengo la kikao hicho ni kutathmini matokeo ya mock,  mbinu na mikakati ambayo itafanyika ili kuongeza ufaulu katika mtihani wa darasa la saba na mitihani mingine.

Pia Mkurugenzi Mtendaji aliwapongeza Walimu wote kwa matokeo mazuri waliyoyapata katika mtihani wa kujipima ( mock)  kanda ya Ziwa ambapo ufaulu umepanda na kufikia asilimia 86 mwaka huu.

"Mwaka jana ufaulu ulikuwa asilimia 79 lakini Mock tumeanza kufika kwenye maeneo ambayo tulikuwa tunayasema asilimia 85 kwa hiyo mimi niwatie shime bado tuendelee kupambana licha ya idadi ya watu waliokuwepo,"

"Tukifika katika ile asilimia kuliyokubaliana mwaka jana ya asilimia 85 ile ahadi tena itajirudia, nia yangu kubwa ya kuja hapa ni kurudia kauli yangu ya mwaka jana tukifika asilimia 85 kwenye tathmini yetu basi ile ahadi yangu ya kuwapeleka Serengeti nitaitekeleza tena ." Alisema Mkurugenzi Mtendaji

Aidha Ndg Mtipa alitoa pongeza kwa Walimu kwa kazi ngumu waliyoifanya licha ya changamoto wanazokutana nazo katika mazingira ya kazi lakini wanapambana ili kusukuma gurudumu la uboreshaji wa elimu.

Awali akitoa taarifa Afisa Elimu ya msingi Wilaya ya Maswa Dkt lucy Kulong’wa alisema Wilaya ya Maswa imefanya vizuri katika mtihani wa mock darasa la saba kwa kuwa ufaulu umepanda kwa asilimia 4.33  kutoka asilimia 80.9 mwaka 2023 na kufika asilimia 85.2 mwaka huu.

Pia  Dkt Kulong"wa alisema Wilaya ya Maswa  imeshika nafasi ya tisa kikanda kati ya mikoa 5 ya Kanda ya Ziwa na kimkoa imeshika nafasi ya tatu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa tapsa Wilaya ya Maswa, ambaye pia ni Mwalimu Mkuu shule ya msingi Shanwa Mwalimu Mbaga Shilla alishukuru  kwa kikao hicho ambacho kimewapa mbinu na mikakati  mbalimbali   ya kuongeza ufaulu kwa sababu kila mwalimu Mkuu atafanya jitihada kuhakikisha kuwa matokeo yanakuwa mazuri.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.