• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC Kaminyoge azitaka Shule zote kusaga Mahindi katika mashine zenye virutubisho

Posted on: November 8th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Mhe. Aswege Kaminyoge  ameagiza Shule zote kusaga mahindi  katika mashine zenye virutubisho ili Watoto wa shule za awali, msingi na sekondari wapate vyakula vyenye virutubisho ambavyo vitawasaidia katika makuzi yao na kuwa na msingi mzuri wa elimu.

Kaminyoge ametoa agizo  katika kikao cha lishe cha robo ya kwanza ya mwaka 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa wilaya kilichohudhiriwa na watendaji wa Kata, wakuu wa Divisheni zinazohusika na masuala ya afua za lishe pamoja na viongozi wa dini.

"Ili utengeneze jamii bora anza na msingi mahususi wa lishe mtu anaweza akaanza awali, akaenda darasa la kwanza akamaliza la saba hajui kusoma na kuandika hata ukimtandika viboko 30 kwa sababu ya kukosa lishe bora, viongozi wa dini wako hapa kutusaidia kuwaambia waumini ili ikifika miaka 20-30 ijayo kizazi hiki kiwe tofauti kinafundishika kutokana na kutumia lishe bora." Amesema Mkuu wa Wilaya

Aidha amewashukuru world vision kwa kuanzisha programu ya kutoa elimu ya lishe kwa akina mama, na watoto ambayo itakuwa kwa kipindi cha miaka saba katika  Kata 25 na Vijiji 50 lengo ni kuhakikisha Watoto chini ya miaka 5 wanapata viini lishe, na akina mama  kuhakikisha wanapata madini chuma.

Katika hatua nyingine  Kaminyonge  alisema vijana barehe wa kike na kiume kuhakikisha  wanapewa elimu na viini lishe ili kuepukana na udumavu.

 Mhe Kaminyoge ameongeza kuwa jukumu kubwa la watendaji wa Kata ni kuhakikisha wanasimamia Watoto wote chini ya miaka 5 na akina mama wanapata  viini lishe  na madini chuma  ambavyo kwa pamoja vitawasaidia kuondoa udumavu kwa watoto katika maeneo yao.

"Tunaposema tumesaini mkataba wa kufuatilia na kusimamia afua za lishe ambao Mhe. Rais aliagiza yanatakiwa matokeo yaonekane matokeo ya kwenye makaratasi yawe na uhalisia, tunaposema akina mama kwenye wilaya yetu hawajifungui watoto wenye mgongo wazi iwe kweli asilimia mia moja hawajifugui watoto hao." alisema  Mhe Kaminyoge.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw. Maisha Mtipa aliwataka watendaji wa kata kufuatilia utoaji wa chakula shuleni kwa kuwa wao ndio wakurugenzi katika maeneo yao hivyo wanawajibu wa kuhakikisha wanasimamia shughuli zote zinazofanyika katika maeneo yao ikiwepo na miradi ya maendeleo.

Bw. Mtipa alisisitiza kuwa suala la lishe lisiposimamiwa vizuri katika jamii litaleta athari katika ukuaji wa watoto ambapo itapelekea changamoto katika  masuala ya makuzi, kutokupata viongozi wazuri kwa sababu jamii isipopata lishe bora watoto wengi watapata udumavu.

"Suala la lishe ni ajenda kuu ambayo Mhe. Rais anaisimamia na ametoa kazi kwa wasaidizi wake ambao ni sisi tulisimamie suala la lishe tusipolisimamia vizuri tutajenga jamii ambayo sio nzuri.''alisema Mkurugenzi Mtendaji

Kwa upande wao viongozi  wa dini wameishauri maeneo ya shule yote yalimwe  kitaalamu kwa kuwatumia maafisa ugani  kwa ajili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ili Watoto wote waweze kupata chakula shuleni ambapo itasaidia kuongeza ufaulu katika mitihani yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.