• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC KAMINYOGE AZINDUA MSIMU MPYA WA UNUNUZI WA ZAO LA PAMBA MASWA

Posted on: May 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amezindua rasmi msimu mpya wa ununuzi wa pamba wa mwaka 2024/2025 katika Wilaya ya Maswa ambapo pamba hiyo itauzwa shilingi 1150 kwa kilo moja ya pamba ikiwa ni bei elekezi kwa mujibu wa Bodi ya pamba Tanzania na kuzitaka AMCOS zote kuhakikisha mizani zao zinakaguliwa na meneja wa vipimo wa  Mkoa wa Simiyu.

“Kama kuna mzani ambao unakuja kufanya kazi katika AMCOS iliyopo katika Wilaya ya Maswa, basi huo mzani upelekwe kwa meneja wa vipimo wa Mkoa hata kama ulikaguliwa nje ya Wilaya ya Maswa kwa sababu kuna baadhi ya makampuni yametoka na mizani Singida na Shinyanga wanakuja nazo kwenye AMCOS zetu.” Mhe Kaminyoge

Pia amesisitiza kuwa mzani wowote ambao haujakaguliwa na Meneja wa vipimo wa Mkoa wa Simiyu utakuwa haujakizi vigezo hivyo hautaweza kudhibitishwa kutumika katika ununuzi wa pamba hata kama umekaguliwa sehemu nyingine.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amesema makampuni yamekubaliana katika kikao hicho kuweka fedha katika akaunti za AMCOS wakati wa ununuzi wa pamba badala ya kuwapa fedha taslimu AMCOS kwa mkataba na AMCOS ihakikishe wananchi wakati wote wanapata pesa wanapouza pamba.

“Ili kuhakikisha tunanufaika na pamba ambayo imelimwa katika wilaya yetu, mkulima anapata kilicho chake, Halmashauri inapata kilicho chake kwa mujibu wa sheria, AMCOS na unioni inapata kilicho chake.” Mkuu wa wilaya

Pia kikao hicho kimekubaliana kuhakikisha kufuta madeni ya AMCOS kwa makampuni, kufuta madeni ya makampuni kwa AMCOS, kufuta madeni ya ushuru kwa Halmashauri ili kuodoa kero hiyo ambayo inatokea ili iishe kabisa.

Kwa upande wake Meneja wakala wa vipimo Simiyu Ndg Francis G. Olwero amewataka AMCOS kuhakikisha mizani zao zimekaguliwa hata kama mizani zao zitakuwa zimekatiwa risiti ili kuona kama inapima vizuri.

Pia amewasisitiza wanunuzi wasinunue mizani bila kufuata ushauri kwa wakala wa vipimo ili kuepuka kukamatwa.

Nae Meneja Mkuu wa SIMCU Simiyu Ndg Fares Muganda amewataka viongozi wa AMCOS kuhakikisha wanachagua viongozi ambao wana weredi ili kujenga heshima kwa AMCOS kwa sababu serikali imewapa heshima kubwa kwa kuwa sasa hakuna SIMIYU MODEL.

“Naamini kabisa Mkuu wa Wilaya kaonyesha kwa dhati jinsi anavyokerwa na hii tabia inayotokea naamini tukipata viongozi wazuri chini ya usimamizi wa mkuu wetu wa wilaya itakuwa ni historia kwa hayo yote yaliyotokea.” Ndg Muganda

Nae Mkaguzi wa pamba Wilaya ya Maswa Ndg Ally Mabruki amesema muongozo kutoka bodi ya pamba Tanzania unawataka wanunuzi wote kununua pamba kupitia vyama vya msingi yaani AMCOS zilizopo katika maeneo husika ambapo amesema pamba yoyote itakayouzwa nje ya mfumo wa vyama vya ushirika  itataifishwa na serikali.

Mkuu wa Divisheni ya kilimo, mifugo na uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Robert Urassa amesema Halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na bodi ya pamba poja na AMCOS imepanga jumla ya vituo 256 ikiwa ni ongezeko la vituo 2 vipya  katika msimu huu hasahasa katika maeneo ya mipaka ya Wilaya jirani ili kupunguza utoroshaji wa pamba iliyozalishwa ndani ya Wilaya ya Maswa.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.