• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC KAMINYOGE AZINDUA BARAZA LA WAFANYABIASHARA MASWA

Posted on: March 26th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amezindua baraza la wafanyabiashara wa sekta ya umma na sekta binafsi  kwa  lengo la kujadili changamoto mbalimbali za wafanyabiashara wa Maswa zinazokwamisha katika kuendeleza biashara zao.

Mhe Kaminyoge amemshukuru Mhe Dkt Samia  Suluhu Hassan  kwa kuhakikisha Tanzania inakuwa na viwanda na hasa  kufikia uchumi wa kati kwa kuboresha na kuweka mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji nchini.

Amesema hayo katika uzinduzi wa baraza la wafanyabiashara wa Wilaya ya Maswa lililofanyika leo tarehe 25 Marchi 2024 na kuhudhuriwa na  wakuu wa taasisi za umma, wakuu wa Divisheni husika, pamoja na wajumbe wa sekta binafsi.

“serikali kupitia Wilaya ya Maswa imehakikisha upatikanaji wa ardhi,  miundombinu ya msingi huduma bora za jamii na kuimarisha  jukwaa la mahusiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi kupitia mabaraza ya biashara.” Mkuu wa Wilaya

Pia ameongeza kuwa baraza lina jukumu la kuhakikisha sekta ya umma na sekta binafsi zinasaidiana ili kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja, uchumi wa familia, uchumi wa kaya, Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Amesema sekta binafsi ni muhimu katika ujenzi wa uchumi wa viwanda katika Wilaya ya Maswa kwa sababu biashara ya uwekezaji inayofanyika  katika Wilaya inaaksi dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 na mpango wa Taifa wa miaka 5 pamoja na mikakati ya Halmashauri na taasisi zote zilizopo katika Wilaya ya Maswa.

Pia amesema baraza hilo ni chombo muhimu kwa ajili ya kukuza na kuendeleza sekta binafsi na uchumi wa Wilaya ya Maswa ambapo Baraza hilo litajadili fursa zilizopo na kutatua changamoto zilizoathiri biashara na uwekezaji.

Ameongeza kuwa hayo ni maagizo ya Mhe Rais kuhakikisha wasaidizi wake  wanasikiliza na kutatua kero za wafanyabiashara pamoja na kuratibu majadiliano katika ngazi ya Wilaya kwa ajili ya kutatua kero ambazo zinakwamisha wafanyabiashara katika kuendeleza biashara zao.

"Ndugu viongozi wa Wilaya ni wajibu wetu kuratibu vikao pamoja na kuhakikisha changamoto zinazoikabili sekta binafsi ya Wilaya yetu pamoja na mapendekezo yatakayowasilishwa na wafanyabiashara yanatekelezwa kwa wakati ili kuboresha Mazingira ya wafanyabiashara." Amesema Mhe Kaminyoge

Amesema adhima ya serikali ya Wilaya ya Maswa ni kuboresha Mazingira ya wafanyabiashara na uwekezaji ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje kwa kuondoa vikwazo vya kibiashara vikiwepo kuondoa tozo zisizo na tija pamoja na kuweka miundombinu yote katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji .


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.