• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC KAMINYOGE AJIANDIKISHA KWENYE ORODHA YA DAFTARI LA WAPIGA KURA WA SERIKALI ZA MITAA

Posted on: October 11th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amewaongoza wananchi wa Maswa katika zoezi la kujiandikisha katika daftari la wapiga kura wa serikali za mitaa ili kupata sifa ya kuwachagua viongozi mbalimbali katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika 27, Novemba 2024.

Mhe.  Kaminyoge amejiandikisha leo tarehe 11, Oktoba 2024 katika kituo cha uandikishaji kilichopo Chuo cha Ufundi Stadi Binza njiapanda ya Lalago   katika Kitongoji cha Mwantoja, Kata ya Nyalikungu Wilayani Maswa Mkoani Simiyu.

Pia Mkuu wa Wilaya amewaomba   wananchi wote wenye sifa ya kuandikishwa katika Wilaya ya Maswa wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika vituo vya kupigia kujiandikishia katika vitongoji 510 vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

“Niwaombe wananchi wote jitokezeni kwa  wingi kujiorodhesha kwa sababu ni haki ya kikatiba ya kila raia mwenye sifa ya kujiandikisha  aweze kupiga kura kwa mujibu wa sheria kwa sababu viongozi wa serikali za mtaa ndio msingi wa viongozi katika nchi yetu.” Ameeleza Mkuu wa Wilaya

Aidha amesema wananchi watakaojiandikisha ni wale wote waliofikisha miaka 18 na kuendelea, awe mtanzania na awe na akili timamu.

Pia Mkuu wa Wilaya amesisitiza kuwa wananchi wanatakiwa kujiandikisha kwenye kitongoji husika ili wawe na nafasi ya kuwachagua viongozi wao  wa serikali za mitaa katika uchaguzi utakaofanyika tarehe 27 Novemba 2024 ambapo watawachagua Mwenyekiti wa kitongoji husika, Mwenyekiti wa serikali ya kijiji, wajumbe wa serikali ya kijiji na wajumbe wa viti maalumu wa serikali za vijiji.

“Mjitokeze kwa wingi kujiandikisha ili mchague viongozi ambao ni wachapakazi wenye uwezo wa kuwongoza wananchi kwenye shughuli za maendeleo na mambo mbalimbali katika maeneo yao.” Amesema Mhe Kaminyoge

Kwa upande wake msimamizi wa uchaguzi Halmashauri Wilaya ya Maswa Ndg. Maisha Mtipa amesema katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Kuna watu zaidi ya laki nne lakini katika zoezi hilo wanatarajia kuandikisha Zaidi ya wananchi laki mbili katika  daftari  la wapiga kura ambalo limeanza leo terehe 11- 20 Oktoba 2024  na kuhitimishwa tarehe 20.10.2024.

Pia Ndg. Mtipa amesema vituo hivyo vinapatikana katika Kila kitongoji ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ina vitongoji 510 ambapo vitongoji 40 vipo katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Maswa.

Aidha  ametoa wito kwa wananchi  wote kuhakikisha wanajiandikisha katika daftari la wapiga kura ili wakati wa Uchaguzi wasikose sifa ya kuchagua viongozi wanaowataka wakati wa kupigia kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika27, Novemba 2024.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.