• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC KAMINYOGE AISHUKURU MAHAKAMA KWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MISINGI YA HAKI

Posted on: February 2nd, 2024

Mkuu wa wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Mhe. Aswege Kaminyoge ameishukuru Mahakama na vyombo vingine vya kutoa haki jinai kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kutoa elimu na haki kwa kuzingatia misingi ya haki ili wananchi wapate haki stahiki.

Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo katika kilele cha wiki ya sheria iliyofanyika katika viwanja vya mahakama yenye kauli mbiu ya “ Nafasi ya Mahakama, wadau umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa taifa, nafasi ya Mahakama na wadau katika kuboresha mfumo jumuishi wa haki jinai”.

Mhe. Kaminyoge  amesema elimu inatakiwa kutolewa zaidi kwa wananchi ili wasitumie pesa nyingi kwa ajili ya manufaa ya familia zao kwa  makanjanja ambao hawana kesi  wanazunguka kuanzia asubuhi mpaka Mahakama inapofungwa kudaka watu kwa ajili ya kuwarubuni vitu mbalimbali kwenda kwa mahakimu.

Tukiweza kufanya hivyo wananchi wetu watakuwa na furaha kubwa katika nchi yao.

 “Leo hii tuna viongozi wa Dini, wananchi mbalimbali, watumishi mbalimbali wana wajibu wa kuhakikisha mahali walipo wanatoa maamuzi yenye haki kwani vitabu vya Dini; Biblia na Msahafu vinazungumzia juu ya utoaji wa haki.” amesema Mhe Kaminyoge

Aidha Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema viongozi wamepewa mamlaka na Mhe. Rais na wananchi kwa ajili kutoa haki ambapo kila mtu ajitafakali anapotoa haki ajiulize je? Ametenda haki au hajatenda haki? hivyo amewataka watumishi na mahakimu  kutoa haki ili mwananchi akitoka Ofisini au Mahakamani apite kifua mbele akisema haki imetendeka.

“Niwaombe waheshimiwa Mahakimu, Wapelelezi, Wachunguzi, TAKUKURU, Magereza Wananchi wanawategemea sana; Mahakimu Mahakama zinawategemea sana kwa ajili ya kutoa haki tufanye kazi kwa kuzingatia misingi ya haki.” Amesema Mkuu wa Wilaya

Pia amemshukuru Mhe. Hakimu kwa kazi kubwa aliyoifanya katika wiki ya sheria ambapo wananchi wengi wamepata elimu ambayo itawasaidia kupata haki iliyo sahihi hivyo ameitaka Mahakama isichoke kutoa elimu kwa wananchi.

Kwa upande wake Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Maswa Mhe. Enos Misana amesema maadhimisho ya wiki ya sheria yamehusisha utekelezji wa shughuli mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kwa umma kuhusiana na masuala mbalimbali ya kisheria, upokeaji wa shida, malalamiko, maoni, mapendekezo mbalimbali  kuhusiana na huduma zitolewazo  na Mahakama.

Ameongeza kuwa zoezi la utoaji elimu kwa umma lilitekelezwa katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya ambapo wananchi na wadau waliweza kujitokeza kupata elimu ya masuala ya kisheria, kuwasilisha malalamiko pamoja na kufungua mashauri kwa njia ya mtandao.

Aidha Hakimu Mfawidhi amesema malalamiko mengi yaliyotolewa yanaeegemea zaidi upande wa ardhi, ndoa, mirathi na utelekezwaji wa watoto ambapo elimu hiyo imetolewa maeneo mbalimbali ikiwepo Shule za Sekondari na maeneo ya minadani.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.