• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC KAMINYOGE AGAWA SARE KWA WAGANI KILIMO 39 WA MASWA

Posted on: August 20th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amegawa sare  kwa Maafisa Ugani 39 wa Wilaya ya Maswa  tarehe 20 Agosti 2024 eneo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imetoa sare hizo kwa lengo la kuwawezesha maafisa ugani hao kufanya kazi kwa ufanisi katika maeneo yao ya kiutendaji ili kuongeza tija katika uzalishaji.

Mkuu wa Wilaya amewataka maafisa ugani wote kuhakikisha wanawafikia wakulima ili kuwapa utaalamu kwa kuwa tayari wana vitendea kazi ambavyo vitasaidia kutoa utaalamu kwa wakulima.

"Rai yangu kwenu ni kuhakikisha mnachukua nafasi hii kumzawadia Mhe Rais, kumheshimisha Mhe Rais katika hivi vitendea kazi alivyovigawa, matokeo ya uzalishaji katika msimu ujao yaongezeke maradufu kama sio mara tano kwa sababu hatuna nafasi ya kusingizia pikipiki wote 39 mnazo, vitendea kazi vingine mnavyo. Hakuna sababu nyingine ya Afisa yeyote, mtaalamu au kiongozi yeyote akipita kwenye maeneo yenu ya kazi akute mazao yapo chini ya kiwango." Amesema  Mhe. Kaminyoge

Ameongeza kuwa Maafisa Ugani hao wanatakiwa kutoa Elimu kwa wananchi kuhusu kanuni bora za Kilimo ili uzalishaji wa mazao uwe na tija ambapo katika zao la pamba uzalishaji utoke kwenye kilo 250 hekari moja mpaka uzalishaji ufikie kilo 1000 hadi kilo 2500 kwa hekari moja.

Aidha Mkuu wa Wilaya amemshukuru Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa anazozifanya katika kukuza na kuimarisha sekta ya kilimo.

Pia ametoa pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya kwa namna alivyojipanga ili kuhakikisha Wilaya ya Maswa inazalisha mazao mbalimbali kwa tija yakiwemo mazao ya kimkakati kama zao la pamba, alizeti na mazao mengine.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amewataka Maafisa Ugani hao kuanzisha vipando vya mazao mbalimbali ili wananchi waweze kujifunza namna bora ya kilimo  ambacho kitaleta tija.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg. Maisha Mtipa amesema Wizara ya Kilimo imejipanga kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya Kilimo ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao mbalimbali ambapo Wizara ya Kilimo imejikita kuleta vifaa ili kuweza kuboresha uzalishaji.

Pia Ndg. Mtipa amewataka Maafisa Ugani kilimo kuhakikisha wanavaa sare hizo wakati wakitekeleza majukumu yao kwa wananchi na katika maeneo yao ya kazi.

Hapa chini ni picha mbalimbali wakati Mhe Mkuu wa Wilaya akikabidhi Sare kwa Wagani Kilimo






Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.