• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC azindua zoezi la upandaji miti Maswa

Posted on: November 10th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge ameipongeza Halmshauri ya Wilaya ya Maswa kwa kutenga bajeti ya shilingi milioni 70 kwa ajili ya kuanzisha kitalu cha miche mbalimbali ambayo itapandwa katika taasisi mbalimbali za serikali na watu binafsi ili kurudisha uoto wa asili na kuhifadhi mazingira.

Mhe.  Kaminyoge Alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa zoezi la upandaji miti katika wilaya ya maswa kwa mwaka 2023/2024 ambalo lilifanyika katika Shule ya Sekondari Zanzui iliyopo Kata ya Zanzui, ambapo zaidi ya  miti 600 ilipandwa katika eneo la shule hiyo.

Pia ameongeza kuwa katika Wilaya ya Maswa kuna tatizo la ukame kutokana na   uharibifu wa mazingira ambao unatokana na ukataji wa miti hivyo amewata viongozi pamoja na wananchi kuwa jukumu kubwa lililopo ni kuhakikisha uoto wa asili unarudi katika Wilaya ya Maswa.

“Msingi mkubwa wa utunzaji wa mazingira ni kuhakikisha tunapanda miti, miti tukiipanda ndio itakayoturejeshea hali nzuri ya tabianchi Mhe. Rais ametuagiza viongozi wote katika ngazi mbalimbali kuanzia Kitongoji, Kijiji, Kata na Wilaya kwa  ujumla wake kuhakikisha kila msimu wa mvua unapoanza tupande miti milioni moja na laki tano kwa mwaka.”alisema kaminyoge

Mkuu wa Wilaya ametoa maelekezo kwa Mkurugenzi  Mtendaji na wananchi kuhakikisha miti inapandwa kama alivyoelekeza Mhe. Rais hivyo amezitaka taasisi zote kupanda miti ambayo itasaidia wananchi kujifunza kwa vitendo kutokana na miti ambayo watakuwa wameipanda.

Pia Mhe. Kaminyoge alizitaka taasisi zote za shule kuandaa vitalu vya miche 20000 kila shule  ili kufikia  lengo la Mhe Rais  la  kupanda miche  milioni moja na laki tano kila mwaka  kwa kuisaidia Halmashauri kujitosheleza  ili  isitafuta miti  kwenye makampuni mengine.

Awali akitoa taarifa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Bw. Maisha Mtipa alisema wametengeneza kitalu chenye jumla ya miti 421000 ambayo itagawiwa katika taasisi mbalimbali za halmashauri ikiwepo vituo vya Afya, Shule za msingi na sekondari pamoja na Zahanati ili kutunza mazingira.

“Kwa kufanya hivi tunaendeleza sera ya serikali ya utunzaji wa mazingira katika nchi yetu na tukiangalia katika maeneo yetu ya Wilaya ya Maswa maeneo mengi hayana miti, sisi Halmashauri tunafanya juhudi kubwa ya kupanda miti ili tulejeshe uoto wa asili wa eneo la Maswa.”  Alisema Mkurugenzi Mtendaji

Nae wakala wa Misitu Wilaya ya Maswa (TFS) Bw. Fabian Mosha alisema kutokana na changamoto ya ukame iliyopo Maswa, Wilaya imejidhatiti kupanda miti milioni moja na laki tano  ili kuhakikisha kuwa agizo la Rais Dkt Samia Suluhu Hassan linafikiwa katika msimu huu wa mvua wa mwaka 2023/2024.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Zanzui Bw. Juma Selemani alimshukuru Mhe Dkt Samia Suhulu Hassan kwa kuhamasisha nchi kurudisha uoto wa asili kwa kupanda miti hivyo mwenyekiti huyo ameahidi kusimamia miti yote iliyopandwa katika eneo hilo na alisema wataendelea  na zoezi hilo la kupanda miti katika Kijiji hicho.

Kwa upande wake mwanafunzi wa shule ya Sekondari Zanzui Maria Maduhu anayesoma kidato cha tatu wameahidi kuitunza miti hiyo ambayo  itawaletea  faida mbalimbali zikiwepo kupata hewa safi sambamba na kuzuia mmomonyoko wa ardhi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.