• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC awataka viongozi kusimamia watoto wote wenye umri wa kuanza shule waandikishwe

Posted on: November 19th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Mhe. Aswege Kaminyoge ametoa wito kwa viongozi wote kuhakikisha wanasimamia watoto wote waliofikia umri wa kwenda shule kuanzia awali, msingi na sekondari waandikishwe kwa ajili ya kuanza masomo  kwa kuwa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya.

Ametoa wito huo katika kikao cha baraza la Madiwani robo ya kwanza ya mwaka 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya  ya Maswa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, wataalamu pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya.

Mhe Kaminyoge  amesema jukumu hilo la msingi wamepewa maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na vijiji kuhakikisha wanawatumia viongozi wa vitongoji kwa kuwa wao ndio wana majukumu mahususi kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanaenda.

Mkuu wa Wilaya  amewahimiza na kuwasisitiza waheshimiwa Madiwani na viongozi kuwasisitiza  wananchi watoto wote walioandikishwa kuanzia awali, msingi na sekondari wanasimamiwa kikamilifu ili kuhakikisha wanamaliza elimu zao.

"Mhe Rais tangu aingie madarakani hakuna mwananchi yeyote amepitiwa juu ya uchangiaji wa miundombinu Jija Mhe Rais ametoa milioni 548 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi yenye darasa la awali na mikondo 2 kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba yenye madarasa 17". Amesema Mhe. Kaminyoge

Pia Mhe Kaminyoge amesema wataanzisha oparesheni kwa kuwatumia Maafisa Tarafa, Watendaji kuhakikisha watoto wote waliopo nyumbani ambao wamefikia umri wa kwenda shule wanaenda ili kumheshimisha Mhe Rais ambaye ametoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na shule mpya.

Pia Mkuu wa Wilaya amesisitiza Madiwani kusimamia mapato ya Halmashauri ili kufikia lengo la makusanyo ifikapo Juni 2024 iwe ni asilimia 100%  usimamizi wa asilimia 40 ya mapato ya Halmashauri itume kama ilivyopangwa.

 Ikiwa asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu na 30%  katika miradi ya maendeleo pamoja na taarifa za afua za lishe ziwepo kwenye taarifa za Kata  kwa kuwa viongozi wamesaini mkataba ili kutekeleza mpango huo wa lishe kwa akina mama wajawazito kupata madini chuma na watoto chini ya miaka 5 kuepuka udumavu.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Budekwa Mhe. Esther Ng'holongo kwa niaba ya Madiwani wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa kazi kubwa anayoifanya na ameahidi kushirikiana nae katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.