• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC ATAKA MIKATABA ISAINIWE BAINA YA MAKAMPUNI NA AMCOS WAKATI WA UNUNUZI WA PAMBA

Posted on: May 22nd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amewaagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Afisa ushirika na makampuni kuandaa mikataba madhubuti yenye mashiko ya kisheria ambayo itasainiwa na pande mbili baina ya  makampuni na makatibu wa AMCOS wakati  wa zoezi  la  ununuzi wa pamba ili kuepusha upotevu wa Fedha na madeni.

Pia Mkuu wa Wilaya amesema mikataba hiyo ikikiukwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa ikiwepo kupelekwa mahakamani ambapo yeyote atakayekiuka atakuwa ameshitakiwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sio kampuni.

Ametoa maagizo hayo katika kikao cha wadau wa pamba kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa tarehe 20 Mei 2024.

Mhe Kaminyoge pia ameyataka makampuni hayo kutoa taarifa katika ofisi yake kabla ya makabidhiano ya mikataba na AMCOS ili kupunguza mlundikano wa Fedha za makampuni mengi kwa AMCOS moja ambayo haitakuwa na uwezo wa kutoa pamba hiyo.

Aidha ametoa wito kwa makampuni yote kuhakikisha yanapokabidhi Fedha hizo kwa makatibu wa AMCOS lazima wawepo wajumbe wengine wa Bodi ya pamba sambamba na hilo amewataka makatibu wa AMCOS, makarani na wahasibu mikataba yao iwe na uhai ili kutekeleza yale yote yanayotokea kama matatizo na migogoro wakati wa ununuzi wa  pamba.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amezitaka AMCOS zote  ziwe na mashine ya kuhesabia Fedha kwa ajili ya kuhakiki ili kuepusha upotevu wa Fedha ambao unatokea wakati wa makabidhiano bila kuhesabu ambao unasababisha AMCOS kuwa na madeni makubwa.

"Afisa ushirika wewe ndio Mkaguzi wa hapa wilayani hakikisha Kila AMCOS inakuwa na mashine za kuhesabia pesa na hao waliochaguliwa juzi uwafundishe namna ya kutumia hizo pesa." Mkuu wa Wilaya

Aidha Mkuu wa Wilaya amezitaka AMCOS kuwa na ubunifu wa kukopa benki ili wawe na uwezo wa kujiendesha wenyewe  kwa  kufanya biashara na makampuni wakati wa kununua pamba makampuni yawe yananunua pamba kwao na sio kwa mkulima.

Kwa upande wake Mrajisi wa Vyama vya ushirika Mkoa wa Simiyu Ndg. Godfrey Mpepo ameyataka makampuni yote yanayonunua pamba kabla hayajapeleka Fedha kwa AMCOS yatoe taarifa kwa mkuu wa Wilaya kuhusu kiwango Cha Fedha na mzigo wanaouhitaji ili kuepusha mlundikano wa Fedha katika AMCOS moja kwa sababu ya uchache wa pamba.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.