• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DAS AFUNGUA MAFUNZO YA USAMBAZAJI WA MATUMIZI YA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI MASWA

Posted on: March 13th, 2024

Katibu Tawala Wa Wilaya ya Maswa Ndg Athuman Kalagwe amezindua mafunzo ya usambazaji wa matumizi ya matokeo ya sensa ya watu na makazi  kwa watendaji na viongozi mbalimbali yenye  lengo la kuwajengea uwezo kutumia matokeo ya sensa ili yawasaidie katika kutekeleza majukumu yao kwa makini na ubora zaidi katika sera ya upangaji wa mipango.

Amezungumza hayo katika kikao cha mafunzo ya usambazaji wa matumizi ya matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa pamoja na wadau mbalimbali yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

ameongeza kuwa Wilaya ya Maswa imejipanga kuhakikisha  mipango na programu zote  za maendeleo zinapangwa kwa kuzingatia matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

“katika program zetu na mipango ya bajeti ya mwaka 2023/2024 imezingatia matokeo ya sensa na takwimu zingine zinazozalishwa na ofisi ya taifa ya takwimu baada ya kutekeleza maelekezo ya serikali  Wilaya yetu imeweka msisitizo wa matumizi ya matokeo ya sensa kwa lengo la kuhakikisha mipango na program hizo zinajibu changamoto mbalimbali.” Amesema Katibu Tawala

Katibu Tawala ameongeza kuwa Halmashauri ya Maswa ina idadi ya watu 427,864 ambapo wanaume 28,255   na wanawake ni 21,9906 ambapo ongezeko la watu ni sawa na asilimia 2.2%.

amesema wananchi wanatakiwa wapate huduma stahiki kwa wakati na zenye ubora zinazozingatia mahitaji harisi ya wananchi kulingana na idadi yao, jinsia yao na kuzingatia mahitaji maalumu ya makundi mbalimbali katika jamii na hali ya mazingira wanapoishi.

“Mafunzo haya kwetu ni muhimu sana kwa sababu yanatujengea uwezo wa kuyatafsiri na kuyatumia matokeo ya sensa ipasavyo na hatimaye kukuza Uchumi wa Halmashauri yetu, kuongeza upatikanaji wa huduma za jamii kwa wananchi na kuchagiza harakati za wananchi kwa kupambana na maadui watatu  ambao ni ujinga ,maradhi na umasikini.” Ndugu Kalaghe

Katibu Tawala amesema takwimu hizo zimekuja kisayansi kwa kuwa zitasaidia viongozi mbalimbali katika mahitaji mbalimbali katika Kata husika kuangalia namna gani maendeleo yatafanyika.

"Hii ni njia moja ya kisayansi ya sisi kuweza kuleta maendeleo kwenye Wilaya yetu leo hii hatutegemei Mtendaji wa kata tukwambie hebu tuletee Kata yako wangapi hawana choo ukashindwa, hatua gani umechukua ukashindwa wakati kila kitu kinajieleza kwa kuwa kila kitu kimewekwa kisayansi."  Katibu Tawala

Pia amesema takwimu hizo ni kipimo kwa watumishi kwa kuwa wamerahisishiwa na watakuwa na uwezo wa kutatua changamoto hizo na Wilaya haitakuwa na shida kabisa.

 Kwa upande wake mwakilishi wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali Ndg Benedict Mgambi amesema mafunzo hayo ni mfululizo wa mafunzo yatokanayo na matokeo ya sensa ya watu na makazi kwa makundi mbalimbali katika jamii.

Pia amesema mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango kazi wa usambazaji wa mafunzo ya matumizi ya matokeo ya watu na makazi ya mwaka 2022 ambapo hadi sasa mafunzo kama hayo yamefanyika kwa makundi mbalimbali mpaka ngazi za chini.

Mafunzo hayo yatahusisha viongozi wa siasa, dini, mira na desturi asasi za kiraia sekta binafsi, taasisi za elimu ya juu, watu wenye ulemavu, waandishi wa Habari na wananchi wa kawaida.

ameongeza kuwa madhumuni ya kusambasa matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 ni kuwajendea uwezo wadau wote  kwa namna ya kutumia  matokeo hayo katika kutekeleza majukumu yao ya uongozi na utendaji katika serikali kuu  na mamlaka za serikali za mitaa.

“kufanya hivyo kutasaidia kuongeza uwazi na kupanua wigo wa matokeo ya matumizi ya sensa kwa serikali, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla ili kupanga mipango jumuishi kwa maendeleo endelevu.” amesema Mgambi

wa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Ndg Maisha Mtipa amemshukuru Rais kwa kuweza kuwezesha zoezi la sensa kuanzia mpango, wakati wanachukua taarifa kwa kuwa taarifa zimechakatwa na kuletwa katika level ya chini kabisa kwa watendaji wa vijiji.

Pia amewataka viongozi wote kuanzia waheshimiwa madiwani,maafisa tarafa , watendaji wa kata na vijiji kila mmoja apate taarifa hizo kwa ajili ya  kufanyia kazi ili kuleta maendeleo ambayo serikali inayahitaji kwa kuwa mipango yote inaanzia ngazi ya chini

 “Tutakapokuwa tunapanga mipango ya Kijiji takwimu hizi zitatuonyesha watu, huduma muhimu za jamii na mambo mengine yaliyoonyeshwa  nitoe wito kwa kila mmoja wetu aliyepo hapa  tutumie hizi takwimu kwa ajili ya  kuleta maendeleo ya nchi yetu.” Amesema Ndugu Mtipa


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.