• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

CMT MASWA YATOA SHS MILIONI 18 KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA MADAWATI KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI

Posted on: April 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge amekabidhi  madawati  100 katika shule za msingi na viti na meza 200 katika shule za  sekondari wilayani Maswa vyenye thamani ya shs milioni 18 zilizotolewa na Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa  lengo la  kupunguza changamoto ya madawati katika shule zenye upungufu huo.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo tarehe 23 April 2024  katika chuo cha ufundi  stadi Binza  kilichopo Njiapanda ya Lalago Maswa  ikiwa ni sehemu ya kuelekea sherehe za  maadhimisho ya  miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar  uliozaa  Tanzania.

Mkuu wa wilaya amewapongeza Wakuu Wa Idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa baada ya kuona changamoto ya ubungufu wa madawati uliopo na kutoa fedha za matumizi ya shughuli za ofisi zao kwa ajili ya kutengeneza madawati ambayo yatakabidhiwa katika shule zenye upungufu mkubwa.

Pia amezitaka taasisi zingine za serikali TARURA, RUWASA, MAUWASA na taasisi za kifedha vikundi na watu binafsi kuiga mfano huo kwa  kutoa mchango kwa jamii wanapofanyia  kazi ili watoto wapate madawati na kupunguza tatizo hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi Binza Mwalimu Mabula Daniel amesema  Chuo hicho kinatoa kozi mbalimbali ikiwepo kozi ya uselemala hivyo chuo kilipokea shs milioni 18 kutoka Timu ya Menejimenti kwa ajili ya kutengeneza madawati seti 100 kza shule za msingi na seti 200 kwa shule za sekondari ambayo yapo tayari kwa matumizi.

Pia Mwalimu Mabula amesema huo ni mwendelezo wa mpango wa kutengeneza madawati 430 na kazi inaendelea pia ametoa wito kwa taasisi zingine na watu binafsi kujitokeza kuiunga mkono halmashauri ili kusaidia kuondoa tatizo la upungufu wa madawati katika Wilaya ya Maswa.

Kwa upane wake mkuu wa Divisheni ya elimu sekondari  Fidelis Apolinary amesema amepokea viti na meza 200 ambavyo vitagawiwa katika  shule zenye upungufu wa madawati ambazo ni  shule ya sekondari nyongo ambayo imepata vitio na meza 100 na shule ya sekondari mwasayi 100.



Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.