• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

CHANJO YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE YAZINDULIWA MASWA

Posted on: April 21st, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mhe Paul Maige amezindua kampeni ya chanjo ya homa ya mapafu kwa ng'ombe katika wilaya ya Maswa ili kuhakikisha Mifugo inakuwa na afya Bora yenye kuleta matokeo chanya kwa wafugaji na kukidhi vigezo vya kitaalamu katika udhibiti wa magonjwa .

Amesema hayo katika uzinduzi wa chanjo hiyo katika kijiji cha Mwanhegele kilichopo kata ya Nyabubinza wakati akimwakilisha Mkuu Wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge.

Mhe Mwenyekiti amesema serikali kupitia Ilani ya uchaguzi itaendelea kuboresha mifugo kwa kuwa mifugo ikiboreshwa masoko yatapatikana kwa sababu hakuna mwananchi ambaye atataka nyama ambayo haina kiwango.

“Unapojitokeza kuchanja mifugo ambayo unaifuga, unajiweka kwenye nafasi nzuri ya kuwa katika mtandao wa kupata soko la uhakika kwa hivyo wafugaji niwape rai muwe mabalozi kwa wengine ili kuhakikisha mifugo yao wanaichanja” Mhe Maige

Aidha ameongeza kuwa athari ya kutokuchanjwa kwa mifugo hiyo kwa ubora haitafanikisha malengo ya Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025.

Mhe Maige amesisistiza kuwa Mifugo ikipatiwa chanjo, malisho mazuri na maji ya uhakika, mifugo hiyo itakuwa mizuri na kuwa chachu kwa wanunuzi kununua nyama hizo kwa ajili ya matumizi ya nyama kwani itakuwa imekidhi vigezo vyote.

“Naamini ya kwamba chanjo hii ya leo tunayoshiriki tunaiunga mkono serikali kupitia Ilani ya uchaguzi ambayo ilieleza kwamba kwa kipindi cha miaka mitano tutahakikisha kwamba mifugo imeboreshwa na ikiboreshwa mfugaji atapata tija, pia chama cha wafugaji na serikali wameendelea kuchukua hatua kwa kuzielekeza taasisi za kifedha kutoa mikopo kwa wafugaji ili iwepo tija” amesema Mwenyekiti wa Halmashauri

Kwa upande wake Daktari wa Mifugo Wilaya ya Maswa Ndg Charles Msira amesema serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kutekeleza mazoezi mbalimbali ya udhibiti wa magonjwa kwa njia ya chanjo lengo ni kumuinua mfugaji kiuchumi

Daktari Msira ameongeza kuwa udhibiti wa magojwa ya mifugo unatekelezwa kwa kuzingatia sheria ya magojwa ya wanyama namba 17 ya mwaka 2003, kanuni ya chanjo na utoaji wa chanjo ya mwaka 2020 pamoja na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2020-2025.

Aidha kulingana na takwimu za ng'ombe waliopigwa chapa 2017 Wilaya Ya Maswa ina jumla ya ng'ombe 305,640 ambapo lengo la wilaya ni kuchanja ngombe hao kwa asilimia 80 dhidi ya ugonjwa wa homa ya mapafu kwa mwaka 2024 ili kukidhi vigezo vya kitaalamu katika udhibiti wa magonjwa na kwa mujibu wa kanuni ya chanjo na uchanjaji mifugo ya 2020.

Pia  ametoa wito kwa mfugaji yeyote atakayekaidi kupeleka ng'ombe wake kwenye vituo vya chanjo vilivyopangwa hatua kali zitachukuliwa ambapo mfugaji   atatozwa shilingi 5000 kwa kila ng'ombe kwa kuwa ugonjwa huo unaenea kwa kasi na kusababisha maambukizi makubwa ambayo yanapelekea vifo vingi vya mifugo na kuatarisha kufungwa kwa minada hivyo kupunguza pato la Halmashauri na taifa

Nae Diwani wa Kata ya Nyabubinza Mhe. Emmanuel Ndalahwa amewataka wafugaji kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo muhimu la mifugo kupata chanjo kwa kuwa masoko mengi ya nje yanahitaji uthibitisho wa chanjo na huduma zingine zilizotolewa kwa kuwa kazi ya ufugaji ni biashara kama zilivyo biashara zingine.


Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.