• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Balozi wa Pamba atoa kanuni Bora za kilimo cha Pamba Maswa

Posted on: December 12th, 2022

Balozi wa pPamba Tanzania Mhe. Agrey Mwanri ametoa elimu juu ya kanuni Bora za kilimo cha   zao la Pamba kwa viongozi, wataalamu wananchi na watendaji kwa kuwaomba watendaji kuanzia kitongoji mpaka wilaya kuwa na mikakati mizuri na mbinu kwa kufanya wenyewe sio kutumia mwakilishi kwa kuwa kazi hiyo haitakuwa na ufanisi katika utekelezaji wake.

Akitoa elimu hiyo Balozi wa Pamba amesema kuwa elimu hiyo itasaidia wakulima namna bora ya kulima Pamba kwa kufuata taratibu zote za utayarishaji wa mashamba kwa kukata maotea yote,  upandaji wa mbegu za pamba kwa kuzingatia kanuni, kutokuchanganya Pamba na   mazao mengine, kupalilia palizi baada ya siku 21 baada ya Pamba kuota na kupulizia dawa kwa kufuata kanuni nzuri za unyunyuziaji ili kupata  Pamba nyingi ambayo italeta  manufaa.

Mhe. Mwanri amesema mpango wa taifa ni kupata Tani milioni 1 na Mkoa wa Simiyu unatakiwa kuzalisha Tani  500,000 ambazo zitagawanywa katika  Wilaya zote za Mkoa wa Simiyu ambapo Wilaya ya Maswa inatakiwa kuzalisha Tani 130,000 za Pamba kwa kuwa zao hilo limechangia katika mabadiliko ya sayansi na technologia ya kisasa, ajira kwa vijana na mapato ya serikali.

Nae mkuu wa wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amesema zao la Pamba ndio kipaumbele kwa kuwa zao ambalo mkulima anapata kipato cha haraka na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, familia, kaya na wilaya kwa kuwa zao hilo linachangia asilimia 75 ya mapato ya Halmashauri yanatokana na ushuru wa zao la Pamba.

"Nichukue nafasi hii tena kukushukuru Balozi wa Pamba ulifanya kazi kubwa mwaka jana kazi  ambayo wakulima wanaipongeza mpaka leo na  kwa mara ya kwanza mimi kama Mkuu wa Wilaya wakati natembea kukagua maandalizi ya kilimo cha Pamba mwaka jana asilimia 70 ya wakulima wetu walikuwa wanapanda kwa mstari" amesema Mkuu wa Wilaya.

Mhe. Kaminyoge amewasisitiza wataalamu, viongozi na watendaji wakatoe elimu hiyo vizuri kwa wananchi kwa kuwa wananchi ni wasikivu ikiwa viongozi watakuwa wawazi kutoa elimu hiyo ambayo itawawezesha wananchi kutambua kanuni Bora za kilimo cha Pamba.

Robert Urassa Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi amesema kwa msimu huu wa kilimo Wilaya imeweka malengo ya kulima heckta 82,212 lakini mbegu zilizofika zinaweza kulima hecta 122,000 tani 2,459 ukiongeza za kilimo hai ambazo ni Tani 600, aidha wameishukuru bodi ya Pamba na Serikali kwa kuleta mbegu za kutosha maeneo mengi japokuwa kulikuwa na upungufu lakini bodi imeendelea kuleta mbegu na tayari Tani 70 zimeongezwa ili kupunguza changamoto kwa wakulima na amewaomba watendaji na viongozi kusimamia kwa karibu  ili wakulima wetu walime kisasa kufikia lengo la Tani 130,000.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa amesema dhamana waliopewa viongozi ni kuwa na usimamizi madhubuti wa mamlaka za serikali za Mitaa ili kuwe na ufanisi ambao utawezesha huduma ziwe bora kwa wananchi na mapato yatakayopatikana yataboresha maeneo ya kazi na kuwa na tija ya ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.

Balozi wa Pamba Tanzania atakuwa Maswa kwa ziara ya  siku 7 kutembelea Kata 14 za Wilaya ya Maswa ili kutoa elimu ya kilimo bora na kanuni za ulimaji mzuri wa Pamba ambao utaleta tija katika dhahabu nyeupe zinazopatikana hapa Maswa.


Matangazo

  • TANGAZO LA UHAMASISHAJI CHANJO YA MIFUGO January 21, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MASWA

    March 10, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.