• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BAJETI YA SHS BILIONI 3.7 KUBORESHA MIRADI YA MAJI VIJIJINI

Posted on: June 24th, 2024

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira vijijini RUWASA imetenga bajeti ya shs bilioni 3.7 katika mwaka wa 2024/2025 kupitia PforR -IV kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali katika vijiji vya  Wilaya ya Maswa.

Miradi ambayo itatekelezwa kupitia Fedha hizo ni pamoja na  kuongeza huduma za maji kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi wa Ipililo, kuanza ujenzi wa miradi ya Budekwa- Kiloleli, kufanya utafiti Mwabayanda , kutumia chanzo Cha maji Cha Ngongwa kuongeza maji mradi wa Isulilo

Kuboresha upatikanaji wa maji mradi wa Sulu kwa kuchimba kisima Mbaragane, kuongeza mradi kwenda Kijiji Cha Manawa ili wananchi wa Kijiji hicho wapate maji ya ziwa Victoria na kuanza ujenzi wa mradi wa Funika.

 Akifungua mkutano wa wadau wa sekta ya maji katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Aswege Kaminyoge amesema huduma ya maji katika Wilaya ya Maswa inapatikana kwa kiwango kikubwa kwa sababu serikali imetenga Fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maji.

Ameongeza kuwa shs milioni 200 imetengwa katika vijiji vyote ambavyo havina maji vya Budekwa, Mwabaraturu, Mwamashindike , Mpindo na vingine ambavyo vina matatizo ya maji kwa ajili ya kufanya utafiti wa maji ya chini ili wananchi hao wapate maji .

"Baada ya miaka 5 au 4 ijayo Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Maswa itakuwa inapata maji kama huduma ya maji kwa asilimia 100 kwa wananchi wake kwa hiyo ni kazi yetu sisi sote kwa upande wa serikali, viongozi Waheshimiwa Madiwani na viongozi mbalimbali kuwaeleza wananchi kazi kubwa inayofanywa na serikali."

Pia ametoa rai kwa wakuu wote wa taasisi, Mkurugenzi Mtendaji, Wakuu wa idara na sekta watengeneze taarifa ambazo watawakabidhi Waheshimiwa Madiwani ili wakaeleze kwa wananchi mambo yaliyotekelezwa na serikali katika Wilaya ya Maswa.

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Wilaya ya Maswa Mhandisi  Lucas Maduhu amesema RUWASA inaendelea kuboresha huduma ya maji ambapo katika kipindi Cha julai 2019 hadi may 2024  RUWASA imetekeleza miradi mbalimbali yenye thamani ya shs bilioni 9.5 kupitia programu mbalimbali lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata maji Safi na salama.

Aidha katika bajeti ya mwaka 2023/2024 kupitia PforR -IV RUWASA ilitengewa jumla ya shs bilioni 4.9 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji  katika vijiji vya Wilaya ya Maswa ambapo miradi hiyo ipo katika hatua za utekelezaji.

Jukumu kubwa la RUWASA ni kusanifu miradi, kujenga miradi na kusimamia utoaji wa maji kupitia vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya jamii (CBWSOs) na ili CBWSOs  ziweze kujiendesha ni lazima visima vyote vilivyopo vijijini visimamiwe na CBWSOs ili zipate pesa kwa ajili ya matengenezo.



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.