• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Mrejesho |
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini ya Mjini
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Uratibu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Tehama
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi
      • Fedha na Uhasibu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Fedha

Idara ya fedha ni miongoni mwa idara za Halmashauri ya Wilaya zinazounda timu ya menejementi ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa  ambayo inalojukumu la kutoa huduma bora mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwa wananchi na wadau wake. Idara ya fedha inalo jukumu la msingi la kusimamia mapato na matumizi ya fedha za Halmashauri jukumu hili limejengwa na kusimamiwa  pia na sheria mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi wa kila siku kwa kutumia sheria ya fedha namba 6 ya mwaka 2001 na marekebisho yake ya mwaka 2004,Sheria ya fedha ya serikali za mitaa CAP  290 ,Sheria ya bajeti ya mwaka 2015, Mwongozo wa fedha wa serikali za mitaa wa mwaka 2009 (The Local Authority Financial Memorundum of 2009) ,Sheria ndogo za Halmashauri pamoja na miongozo na nyaraka mbalimbali za Serikali zinazosimamia taratibu za fedha.


Katika kutekeleza majukumu yake Idara ya Fedha imegawanyika katika vitengo vikuu kama ifuatavyo:


Kitengo cha Mapato

Kitengo cha Matumizi

Kitengo cha Ufungaji hesabu za mwisho (Final Accounts)

Kitengo cha Mishahara

Kitengo cha Biashara



Kitengo cha Mapato

Kitengo hiki kinasimamia shughuli zote za ukusanyaji wa mapato kwa kushirikiana na Idara zenye vyanzo mbalimbali vya mapato kulingana na bajeti ya Halmashauri ya Mji.

Kinasimamia mfumo wa ukusanyaji mapato ya Halmashauri wa kieletroniki (Local Government Revenue Collection information system-LGRCIS) kwa kufanya yafuatayo:

Kutoa stakabadhi za kukiri mapokezi

Kutunza kumbukumbu zote za vyanzo vya Mapato ya Halmashauri

Kuandaa na kutoa taarifa za makusanyo ya mapato ya Halmashauri  kwa mwezi,Robo mwaka na Mwaka mzima.


Kitengo cha Matumizi

Kitengo hiki kinasimamia shughuli zote zinazohusiana na malipo ya fedha za Halmashauri kama           vile:


Kuandaa hati  za malipo mbalimbali ya Watumishi,wazabuni,na taasisi mbali mbali zilizotoa huduma kwa Halmashauri .

Kusimamia na kutumia mfumo wa malipo wa kielectroniki  (IFMS-EPICOR SYSTEM)

Kutunza kumbukumbu za malipo yote yanayofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.


Kitengo cha Mishahara

Kitengo hiki kinashughulika na masuala ya urekebishaji na ulipaji wa mishahara ya watumishi kwa kushirikiana na idara ya  Utumishi

Kusimamia malipo yanayofanana na ajira kwa watumishi wa muda mfupi hasa wanaolipwa kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.


Kitengo cha Ufungaji wa Hesabu za Mwisho (Final Financial Statements)

Kitengo hiki kinahusika na kuandaa taarifa za fedha za mwaka za Halmashauri (Final Financial Statements)

Kuandaa na kuweka vizuri kumbukumbu zote zinazohusiana na hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Maswa.


Kitengo cha Bihashara

Kitengo hiki ni maalumu kwa ajili ya kusimamia shughuli zote za biashara katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kama vile:

Utoaji leseni zote za kibiashara

Kutoa ushauri katika masuala ya biashara

Usimamizi wa masuala ya utekelezaji wa sheria ya leseni za biashara ya Mwaka 1972



Majukumu ya Afisa Bihashara

Kuratibu na kusimamia  masuala yote ya biashara katika Halmashauri.

Mshauri Mkuu wa masuala ya Sheria za Biashara katika uendeshaji wa biashara.

Mratibu na Msimamizi wa shughuli za utoaji na ukaguzi wa leseni za biashara.

Kuandaa taarifa za utekelezaji wa shughuli mbalimbali za sehemu ya Biashara kwa mwezi,robo na mwaka.

Kuandaa Mpango kazi na bajeti kwa Sehemu ya Biashara.

Kutoa tafsiri ya Sheria na miongozo ya maswala ya Biashara kutoka Serikali Kuu kuja Halmashauri.

Kusimamia kwa karibu na kutoa ushauri wa kitaalamu katika eneo la sekta isiyo rasmi.

Kuratibu, kukusanya na kutunza taarifa na takwimu zinazohusu masuala ya biashara.

Kusimamia utekelezaji wa shughuli za uendeshaji wa biashara na kuhakikisha kwamba viashiria vya utekelezaji vianafikiwa.

Utoaji wa leseni za usafirishaji abiria kwa kutumia pikipiki (bodaboda na bajaji) kwa mujibu wa SUMATRA.

Kufanya usajili wa taxi, Bajaji na  bodaboda zinazofanya biashara ndani ya Halmashauri.

Kufuatilia utekelezaji wa bei za mafuta zinazotolewa na EWURA

Ufuatiliaji wa bei za mazao katika masoko

Kuratibu maonyesho ya biashara ngazi ya Wilaya.

Kusimamia miradi inayotekelezwa kupitia Sehemu ya biashara.



Matangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI June 19, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI May 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO May 30, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WALIMU WA AWALI WAPATIWA MAFUNZO YA MBINU BORA ZA KUFUNDISHIA

    June 10, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST KWA WATAALAMU WA UNUNUZI WILAYANI MASWA

    March 27, 2025
  • DKT ANNEY; NENDENI MKASIMAMIE MIRADI YETU VIZURI

    March 26, 2025
  • VIKUNDI 15 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATA MKOPO

    March 26, 2025
  • Tazama zote

Video

Fursa za uwekezaji Mkoani Simiyu
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sensa ya mwaka 2022
  • Taarifa ya Mapato na matumizi
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa IMIS
  • Mfumo wa PlanRep
  • Government Web Framework
  • Mfumo wa PREM
  • Maswa DC Mail Domain
  • Hotuba ya Mh. Waziri Mkuu PLANREP/FFARS

Viunganishi linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Sekretariet ya Ajira
  • Ikulu
  • Baraza la Mitihani Tanzani
  • Wizara ya Elimu Tanzania
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Mwonekano wa Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Maswa

    Sanduku la Posta: 170, MASWA

    simu ya Mkononi: +255 282 750 271

    Simu: +255 282 750 271

    Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.