Idara ya Ardhi na Maliasili ina shughulika na kazi zifuatazo:-
i.Kuandaa Michoro ya mipango miji.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa imeandaa michoro katika maeneo yafuatayo; Mamlaka ya mji mdogo wa Maswa, Malampaka na Lalago.
ii.Kutoa huduma ya upimaji wa viwanja na mashamba.
Wilaya inayo maeneo matatu (3) yanayohitaji upimaji wa viwanja na huduma nyingine za ardhi, ambayo ni: Mammlaka ya mji mdogo, Malampaka na Lalago. Ukuaji wa miji hiyo unaongezeka kwa kasi siku hadi siku kutokana ongezeko la ujenzi wa viwanda vya pamba na idadi ya watu kuhamia mijini. Ongezeko hili ambalo limeinua kipato linasababisha mahitaji ya viwanja vya kuishi na matumizi mengineyo.
Maombi ya viwanja Zaidi ya 700 yanapokelewa kwa mwezi. Mamlaka ya mji mdogo wa Maswa kuna viwanja 4,872, Malampaka viwanja 650, na Lalago viwanja 300 Jumla ni viwanja 5,822. Malengo ya mwaka wa fedha 2015/2016 ni kupima viwanja 1,250 Mamlaka ya mji mdogo wa Maswa, Malampaka viwanja 530 na Lalago viwanja 250.
Idara ina mashamba 3,674 yaliyopimwa na kutolewa hati za kimila na hati za mijini 1,500 zimetolewa.
iii.Kusimamia utunzaji wa mazingira na uoto wa asili.
Idara pia inahusika kutoa huduma za ugani kwa Wilaya nzima katika masuala ya upandaji miti na hifadhi ya mazingira hasa utunzaji wa vyanzo vya maji. Maofisa ugani wanatoa huduma ya elimu ya kuhifadhi mazingira hususani upandaji miti na kutunza ngitili.
Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Sanduku la Posta: 170, MASWA
simu ya Mkononi: +255 282 750 271
Simu: +255 282 750 271
Barua Pepe: ded@maswadc.go.tz
Copyright ©2022 Maswa District Council. All rights reserved.